.

Chanzo cha picha, Facebook

Maelezo ya picha, John Heche

    • Author, Leilah Mohammed
    • Nafasi, BBC Swahili

Iwapo wewe ni mgeni katika ukanda wa Afrika ya Mashariki basi ninapotaja majina haya mawili , ni vigumu kuelewa kwa nini yametajwa katika sentensi moja.

John Heche na Edwin Sifuna, wametengwa na mipaka ila kimsingi viongozi hawa wawili huenda wakatajwa kama pacha wa siasa za uwajibikaji katika mataifa yao binafsi na vile vile Afrika Mashariki.

Unaweza kujiuliza ni kwa nini mwandishi huyu aliamua kuwaweka wawili hawa kwenye kapu moja, vuta kiti nikupe maelezo kisha utafanya uamuzi ikiwa wana tofauti nyingi zaidi ya wanavyofanana.

Pia unaweza kusoma

Ujana na uongozi wa siasa pinzani

Edwin Sifuna ambaye ni Seneta wa jimbo la Nairobi nchini Kenya, ni moja wapo ya Makatibu wakuu wenye umri mdogo katika chama kikubwa cha upinzani nchini Kenya – ODM. John Heche naye ni mbunge wa zamani wa eneo bunge la Tarime nchini Tanzania – na kwa sasa yeye ndiye Naibu mwenyekiti wa chama kikubwa cha upinzani Tanzania – CHADEMA.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *