.

Chanzo cha picha, Getty Images

    • Author, Tessa Wong
    • Nafasi, BBC Reporter

China imezindua idadi kubwa ya silaha mpya, ndege zisizo na rubani na vifaa vingine vya kijeshi katika gwaride kubwa ambalo waangalizi wengi wanaona kuwa ni ujumbe wa wazi kwa Marekani na washirika wake.

Katika hafla hiyo, Rais Xi Jinping aliwakaribisha zaidi ya wakuu 20 wa nchi za kigeni, akiwemo Rais wa Urusi Vladimir Putin na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, ambao wote wanaitegemea China kwa msaada wa kiuchumi na mwingine.

Gwaride hilo lilikuwa ni onyesho la kuimarika kwa uwezo wa Bwana Xi duniani, pamoja na uwezo wa kijeshi wa China, na ulikuwa na kombora la “Guam Killer”, ndege isiyo na rubani ya “Loyal Companion” na hata mbwa mwitu wa roboti.

Lakini zaidi ya vishindo na silaha mpya, tulijifunza nini kutokana na sherehe hiyo?



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *