Taifa ya Stars ya Tanzania ilishindwa kutamba mbele ya Nigeria na kukubali kichapo cha shingo upande cha magoli 2-1.

Uganda The Cranes wenyewe walijikuta kwenye hali mbaya zaidi kwa kubamizwa goli 3-1 walipokwaana na Tunisia mjini Rabat.

Hata hivyo, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imewapa matumaini ya awali mashabiki wa soka wa Afrika Mashariki na Kati kwa ushindi wa kupapatua wa bao 1-0 mbele ya Benin.

Kwenye mechi nyingine, timu ya taifa ya Senegal au Simba wa Teranga, walikunjua makucha na kuwararua bao 3-0 vijana wa Botswana.

Hii leo mechi za ufunguzi wa hatua ya makundi zinamalizika kwa michezo minne ikiwemo itayaowakutanisha Ivory Coast dhidi ya Msumbiji na Algeria itakuwa na miadi na Sudan.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *