Ulinzi mkali umewekwa pamoja na jiji kufungwa kabisa. Uchaguzi huu unafanyika wakati taifa hilo likijaribu kujinasua kutoka kwenye miongo ya migogoro, likikabiliana na uasi wa wanamgambo wa Al-Shabaab na pia majanga ya asili ya mara kwa mara.

Zoezi hilo linatajwa kama jaribio la mfumo wa upigaji kura wa moja kwa moja unaoungwa mkono na Rais Hassan Sheikh Mohamud, ingawa limekumbwa na upinzani kutoka kwa majimbo, wanachama na vyama vikuu vya upinzani ambavyo vimeususia uchaguzi.

Takribani wagombea 1,600 wanashindania viti 390 vya halmashauri katika eneo la Banadir, huku wapiga kura wapatao 400,000 wakitarajiwa kushiriki.

Kwa mujibu wa mamlaka za uchaguzi, usafiri wote utasimamishwa siku ya kura, uwanja mkuu wa ndege utafungwa, na zaidi ya maafisa 10,000 wa usalama watapelekwa kulinda zoezi hilo.

Uchaguzi huu unatajwa kuwa wa kihistoria, lakini wachambuzi wanaonya kuwa mvutano wa kisiasa na hali ya usalama vinaweza kuathiri mustakabali wa demokrasia nchini Somalia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *