Kauli ya Putin inajiri baada ya shambulio kubwa la droni na makombora kutoka Urusi, lililomfanya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy kusema kuwa Urusi inaonyesha nia ya kuendeleza vita ilhali Kyiv inataka amani.

Zelenskiy anatarajiwa kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump huko Florida leo Jumapili kutafuta suluhisho la vita ambavyo Putin alivianzisha takriban miaka minne iliyopita.

Wakati huo huo, Urusi imedai kuiteka miji kadhaa katika mikoa ya Donetsk na Zaporizhzhia, madai ambayo Ukraine imeyakanusha, ikisema mapigano bado ni makali na operesheni za ulinzi zinaendelea.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *