Shirika la Umoja wa Mataifa linalishughulikia wahamiaji lilisema siku ya Alhamisi kuwa watu wasiopungua 285 walikuwa miongoni mwa wale waliondoka katika makazi yao kwenye kipindi cha siku mbili huko mji wa Kadugli na Al-Kuwaik Jimbo la Kordofan Kusini kutokana na hali mbaya ya usalama.

Katika taarifa, Shirika la Kimataifa la Wahamiaji (IOM) linasema maafisa wake wamethibitisha watu 85 wameondoka Kadugli, mji mkuu wa jimbo hilo, kutokana na ukosefu wa usalama na operesheni ya kijeshi Januari 27 na 28.

Shirika hilo limeongexa kuwa watu wengine 200 waliondoka katika makazi yao siku ya Jumatano eneo la mji wa Al-Kuwaik sehemu ya Mashariki huko Kordofan Kusini, pia ikitajwa sababu ya kutokuwa na usalama kama chanzo cha kuondoka kwao.

Kulingana na IOM, familia hizo zilielekea katika jimbo la White Nile kusini mwa Sudan na eneo la Kelik katika jimbo jirani la Kordofan Magharibi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *