Mawaziri 27 wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wamekutana Alhamisi, Januari 29, kujadili hali katika eneo la Maziwa Makuu, na haswa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kufuatia ombi la Ubelgiji, kwa uungwaji mkono wa Ufaransa, la kuiweka DRC kwenye ajenda, nchi sita za Ulaya zilielezea kuunga mkono kwao hatua kali zaidi za Ulaya katika mgogoro huu, zikitaka kuimarisha ushiriki wa kidiplomasia nchii DRC na kuunga mkono juhudi za utulivu wa kikanda.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Brussels, Pierre Benazet

Kwa Umoja wa Ulaya (EU), kuongezeka kwa vurugu kunamaanisha kwanza kabisa kuweka chaguzi zote za kidiplomasia mezani ili ziwe na ufanisi ikiwa hali itazidi kuwa mbaya. Kwa hivyo, hakuna suala la kuweka vikwazo, lakini kulingana na baadhi, kuvitumia “kwa muda mrefu” haipaswi kupuuzwa.

Kulingana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ubelgiji Maxime Prévot, hali mashariki mwa DRC ni “mbaya zaidi kuliko hapo awali,” na EU lazima ifanye jitihada zote kwa kutumia uwezo wake kupata njia za kupitisha misaada ya kibinadamu.

“Mwanamke mmoja hubakwa kila baada ya dakika nne, mtoto kila baada ya dakika 30,” waziri wa Ubelgiji alitangaza. “Ni muhimu kufanya kinahowezekana kushinikiza kufunguliwa uwanja wa ndege wa Goma, kwa mfano, ili kutoa msaada huu wa kibinadamu kwa kiwango kikubwa. Bila shaka, hakuna nia ya kutumia uwanja wa ndege kwa madhumuni ya kijeshi. Ahadi ya Ulaya lazima iwe pana zaidi katika kuunga mkono watu ambao wamekuwa wakiteseka na vitisho vya kutisha vya mzozo huu kwa muda mrefu.”

Umoja wa Ulaya (EU), unasema mbali na dharura ya kibinadamu, wakati umefika wa kutathmini uaminifu wao wa kijiografia, haswa katika eneo la Maziwa Makuu. Baadhi wanabainisha mabadiliko ya mbinu yanahitajika, ikimaanisha kwamba Umoja wa Ulaya sasa unapaswa kujiweka kama mshirika wa kidiplomasia na mwezeshaji. Baada ya hapo ndipo litakuja pendekezo la msaada wa kifedha.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *