
Kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim, linalohusishwa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) katika mji wa bandari wa Bandar Abbas ulioko katika Ghuba ya Uajemi, mtu mmoja aliuawa na wengine 14 kujeruhiwa. Mashuhuda pia waliripoti angalau mlipuko mmoja karibu na mji mkuu, Tehran. Katika eneo la kusini-magharibi mwa Iran, kuna taarifa ya mlipuko wa gesi na kusababisha vifo vya watu wanne.Mazoezi ya kijeshi ya majini ya siku tatu yanayoratibiwa na IRGC yanatarajiwa kuanza muda si mrefu katika Ghuba ya Uajemi, ambapo China na Urusi pia zinatazamiwa kushiriki. Na hiyo inakuja wakati Rais wa Marekani Donald Trump ameliweka jeshi pamoja na meli za kubeba ndege za kivita katika eneo hilo la Ghuba.