Kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa kwa niaba ya gazeti la Bild na kuchapishwa leo Jumamosi, iwapo uchaguzi wa shirikisho ungefanyika kesho, asilimia 26 ya waliohojiwa walisema wangeipigia kura Christian Democratic Union (CDU) ya Merz au chama chake ndugu cha Bavaria, Christian Social Union (CSU). Chama cha AfD pia kimekuwa katika kiwango cha asilimia 26 kwa wiki kadhaa, hali iliyokifanya kuwa mbele ya vyama vinavyounda serikali ya muungano. Mara ya mwisho kwa CDU/CSU kuwa sawa na AfD katika utafiti wa INSA ilikuwa mwezi Septemba 2025. Utafiti wa INSA ulifanywa kati ya Januari 26 na 30, ukihusisha watu 1,204 wenye sifa za kupiga kura nchini Ujerumani, na na kiwango chake cha juu cha makosa kitakwimu kikikadiriwa takriban asilimia 2.9.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *