Kwa sasa, ufunguzi huo unafanyika kwa majaribio, na watu hawataruhusiwa kuvuka mpaka hadi kesho, kutokana na majadiliano yanayoendelea kuhusu usalama na taratibu za uendeshaji.

Msemaji wa Israel amethibitisha hatua hiyo, huku vyanzo vya Kipalestina vikisema kuwa wagonjwa takriban 50 ndio watakaoanza kuruhusiwa kutoka Gaza pamoja na walezi wao.

Hata hivyo, vyanzo vya usalama vya Misri vinasema upande wa Palestina bado haujafunguliwa, kwani jeshi la Israel linaendelea kuudhibiti mpaka tangu kusitishwa kwa mapigano mwezi Oktoba.

Ufunguzi wa mpaka huu ni sehemu ya mpango wa amani wa Rais wa Marekani Donald Trump, na unajiri baada ya kundi la  Hamas kukabidhi mabaki ya mateka wa mwisho wa Israel waliokuwa wanashikiliwa Gaza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *