Akizungumza wakati wa mkutano na mwenzake wa New Zealand, Winston Peters, Wadephul alisema Ujerumani haina tatizo na kukubaliana na ukweli na jukumu la Muungano wa Kisovieti kwenye kuushinda utawala wa Kinazi wakati wa Vita vya Pili vya Dunia.

Urusi ilisema hapo awali kwamba sera ya nje ya Ujerumani kuelekea Ukraine inaundwa na dhana ya ulipizaji kisasi, ikiituhumu Berlin kwa kuishi na andasa za kurekebisha mambo iliyoyapoteza kwenye historia yake.

Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano wa kila mwaka wa waandishi wa habari wa Waziri wa Mambo ya Nje Sergei Lavrov, Urusi ilisema uungaji mkono usio masharti kwa Ukraine una ajenda ya kulipiza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *