Jeshi hilo linaselam limewauwa wanamgambo 216katika mashambulizi yaliyoulenga mkoa huo wa kusini magharibi. Jeshi hilo vile vile limesema kuwa walinda usalama 22 na raia 36 waliuwawa katika mashambulizi hayo.

Shughuli huko Balochistan ambao ndio mkoa mkubwa na maskini zaidi wa Pakistan, zilisimama Jumamosi iliyopita baada ya waasi wa Jeshi la Ukombozi la Baloch, BLA, kuvamia mashule, benki, masoko na vituo vya usalama kote katika eneo hilo, katika mojawapo ya operesheni zao kubwa kufanyika.

Mkoa wa Balochistan ulio na utajiri wa madini unapakana na Afghanistan na Iran, na kwa miongo kadhaa umekabiliwa na mashambulizi ya waasi hao wanaotaka kujitawala na mgao mkubwa wa maliasili za eneo hilo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *