
Taarifa kutoka kwa maafisa wa usalama wa Uturuki zinasema kwamba Uturuki imeongeza uwepo wake wa kijeshi nchini Somalia, ikiwa ni pamoja na kupeleka vitengo vya anga na ardhini vinavyolenga kusaidia taifa hilo la Afrika Mashariki katika mapambano yake dhidi ya ugaidi, huku mashambulizi yakiendelea kuongezeka jijini Mogadishu na mikoa yake jirani.
Kikosi cha Pamoja cha Somalia-Uturuki na Kamandi ya Kitengo cha Anga cha Uturuki vinaendelea kuimarisha uwezo wa Somalia wa kupambana na ugaidi kupitia msaada wa kijeshi, mafunzo, na ushauri wa kitaalamu, wamesema maafisa wa usalama wa Uturuki siku ya Alhamisi.
Kamandi ya Kitengo cha Anga cha Uturuki nchini Somalia imeimarishwa kwa kuongezwa kwa vitengo vipya, na rasilimali mpya zilizowekwa pia zitsaidia katika operesheni za kupambana na ugaidi nchini Somalia, wanasema.
Mapambano ya Somalia dhidi ya Al-Shabaab
Somalia imekuwa ikipigana na Al-Shabaab, kundi la kigaidi linalohusiana na Al-Qaeda, kwa zaidi ya muongo mmoja.
Licha ya shinikizo la kijeshi lililodumu kutoka kwa majeshi ya Somalia, vikosi vya Umoja wa Afrika na washirika wa kimataifa, kundi hili linaendelea kutekeleza mashambulizi ya kigaidi, hasa jijini Mogadishu na mikoa ya jirani.