KAGERA; WAKALA wa Barabara (TANROADS) na wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura), wamekutana na wadau mbalimbali wa barabara wakiwemo wabunge mkoani Kagera.
Kikao hicho kilikuwa maalumu kwa ajili ya kuwasilisha rasimu ya bajeti ya kutengeneza barabara na madaraja kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kagera, Joel Samwel, amesema wanakadiria kutumia Sh bilioni 14.5 kwa mwaka huo kwa ajili ya matengenezo ya barabara na madaraja, ingawa bajeti halisi inayoweza kutosheleza vizuri barabara za mkoa wa Kagera ni Sh bilioni 25.8.

Kaimu meneja wa TARURA Mkoa wa Kagera, Mahona Njigela amesema wanakadiria kutumia Sh bilioni 23.7 kwa ajili ya matengenezo ya aina mbalimbali ya barabara, vivuko na madaraja, ili kusogeza huduma ya usafirishaji kwa wananchi
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahya Kido, amewaagiza TANROADS na TARURA mkoani humo kuzingatia na kutoa kipaumbele katika masuala ya ajira kwa vijana na wanawake, wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoendelea na inayotarajiwa kutekelezwa.