
HUDUMA za usafiri zimekumbwa na kadhia katika maeneo ya Marangu, Holili, Njiapanda na Mwanga baada ya madereva wa daladala kuanza mgomo leo asubuhi. Mgomo huo, ulioanza majira ya saa tatu asubuhi, umepelekea abiria wengi kutafuta usafiri huku wengine wakilazimika kutafuta njia mbadala ili kufika kazini au shule.
Madereva wanasema sababu ya mgomo ni kupinga bajaji kupakia abiria katika vituo vyao vya daladala, jambo linalopunguza wateja wao na kuathiri mapato ya kila siku. “Bajaji wamekuwa wakipakia abiria kwenye vituo vyetu, hivyo tunashinikiza mamlaka kuchukua hatua mara moja,” alisema kiongozi wa madereva wa daladala.
Mgomo huu umekwamisha usafiri katika miji midogo na vijiji, huku mamlaka za usafiri zikisubiri hatua zinazochukuliwa na pande zote husika. SOMA: Daladala zapigwa ‘pini’ unyanyasaji wanafunzi Dar