- Gavana wa Kaunti ya Machakos, Wavinya Ndeti, amezua vicheko mtandaoni baada ya video kumuonyesha akihangaika na Kiingereza wakati wa hotuba yake ya kaunti
- Video hiyo ilimuonyesha akigugumia na kukwama katika kusoma hotuba yake iliyoandaliwa, jambo lililozua maoni mseto kutoka kwa watu
- Mitandao ililipuka kwa maoni, huku baadhi wakikumbuka kauli yake maarufu ya “yaliyo ndwele sipite” na kushangaa kwa nini hadhira ilikuwa inamshangilia licha ya makosa hayo
Mnamo Jumatano, Februari 26, Wavinya aliandaa kile alichokiita hotuba ya hali ya kaunti, akielezea viongozi na wakazi kuhusu miradi inayoendelea.

Source: Facebook
Mnamo Jumatano, Februari 26, Wavinya aliandaa kile alichokiita hotuba ya kaunti, akitoa maelezo kwa uongozi na wapiga kura kuhusu miradi inayoendelea.
“Kwa dhati ninawashukuru wakazi wa Kaunti ya Machakos waliojitolea kufuatilia hotuba ya Hali ya Kaunti nje ya majengo ya Bunge la Kaunti ya Machakos, pamoja na wale waliofuatilia kupitia vituo vya habari vya humu nchini na majukwaa mbalimbali ya mitandao ya kijamii.

Pia soma
Tabitha Karanja: Seneta wa Nakuru amshtua Jeff Koinange baada ya kufichua kuwa yeye ni bilionea
Ninathamini sana uungwaji mkono wenu na ninaahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa ustawi wa watu wa Machakos na maendeleo ya kaunti yetu,” aliandika baadaye.
Je, Wavinya Ndeti alihangaika kusoma Kiingereza?
Hata hivyo, hotuba hiyo haikuwa laini. Kipande cha video kinaonyesha Wavinya akigugumia na kukosea matamshi ya maneno ya Kiingereza.
“Mheshimiwa Spika na wajumbe waheshimiwa. Maono yangu ya vituo vya kisasa vya utawala yanatimia. Tumeidhinisha tovuti kwa ajili ya taasisi za kiwango cha kimataifa, ikiwa ni pamoja na uchunguzi wa ultrasound – samahani,” aliomba radhi.
Alisema alitaja “ultrasound” kwa sababu alikuwa akifikiria kuhusu hospitali.
“Ultra… ultramodern football…” alisema kabla ya kunong’ona bila kuweza kusoma neno lililofuata.
Kisha alionekana kuchanganyikiwa kwa muda mfupi.
Alisimamisha hotuba ili kujaribu kufasiri maneno yaliyokuwa mbele yake huku akiyaangalia kwa makini.
“Decentralised…” alisema lakini akakwama tena.
“Madam Speaker,” alianza upya, lakini akasimama na kupepeta karatasi zake.
Alipata sehemu nyingine ya hotuba na kuendelea kusoma, lakini hali ileile ikajirudia.
“The Department of Works has been operating from a condemned building in demoted… demotivated…” alisoma kabla ya kukwama ghafla tena.
Kisha aliinua macho, akionekana kukata tamaa lakini akitabasamu, na kunywa maji huku umati uliokuwepo ukimpigia makofi.
Katika sehemu ya maoni, watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii walishangazwa na changamoto zake za Kiingereza, huku wengine wakikumbuka msemo wake maarufu wa “yaliyo ndwele sipite,” ambapo alichanganya msemo sahihi “yaliyopita si ndwele.”
Wakenya walisema nini kuhusu Kiingereza cha Wavinya Ndeti?
Onlylitboyofficial: “Huyu angejenga tu barabara ya kwenda kwake.”
trapkid__alvin: “Hii ni mbaya, nina uhakika alitokwa na jasho sana.”
boy_shebe254: “Mungu wa Kioko yuko kazini.”
0nlymoh1: “Yaliyo ndwele sipite haikuwa mzaha?”
mconditisam254: “Mbona wanapiga makofi kila anapokunywa maji?”
Wavinya Ndeti alisema nini kuhusu Sammy Kioko?
Kwingineko, mjasiriamali Sammy Kioko alijibu madai kutoka kwa serikali ya Kaunti ya Machakos kwamba alikuwa akichafua jina la Wavinya.

Source: Facebook
Kioko alisema anadai KSh milioni 19 kwa kazi ya urembeshaji (embroidery) aliyofanya kwa kaunti hiyo. Baada ya kushindwa kupata usikivu wa gavana, aliweka kambi nje ya ofisi yake.
Kaunti ilikanusha deni hilo, ikisema hakukuwa na mkataba wowote na kudai kwamba Kioko hakuwa msambazaji aliyesajiliwa. Kioko naye alishiriki nyaraka kuunga mkono madai yake.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke

