Waombolezaji nchini Israeli siku ya Jumatatu (Machi 30) walishiriki kwenye mazishi ya mwanajeshi wa IDF aliyeuawa katika shambulio la wapiganaji wa Hezbollah kutoka nchini Lebanon.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Sergenti Liran Ben Zion, mwenye umri wa miaka 19, aliuawa kwenye mapigano Kusini mwa Lebanon.
Lebanon iliingia kwenye mzozo unaoendelea mashariki ya kati Machi 2 baada ya wapiganaji wa Hezbollah wanaoungwa mkono na Iran kurusha makombora kuelekea Israeli.
Hezbollah walisema walichukua hatua ya kuishambulia Israeli kujibu mauaji ya kiongozi wa kiroho wa Iran Ali Khamanei aliyeuawa katika mashambulio ya Israeli na Marekani.
Tangu wakati huo, Israeli imewaagiza wakaazi wa kusini mwa Lebanon kuondoka, ikitekeleza mashambulio na oparesheni kwenye eneo hilo katika kile inasema ni juhudi zake na kupambana na wapiganaji wa Hezbollah.