Masoko ya hisa ya Asia yameshuka siku ya Jumatatu wakati bei ya mafuta ikipanda tena, huku bei ya mafuta ghafi ya WTI, kiwango cha Marekani, ikizidi tena kizingiti cha dola 100.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mapema asubuhi ya Jumanne (Machi 31), pipa moja la mafuta liliuzwa kwa dola 115.17 za Kimarekani kwenye masoko ya Asia, ikiwa ni muda mchache baada ya meli nyingine ya mafuta, Al Salmi, kushambuliwa kwenye bandari ya Dubai.

Meli hiyo ilikuwa imebeba mapipa milioni mbili kutokea Kuwait na Saudi Arabia na mamlaka za Dubai zinasema zinaendelea na juhudi za kuuzima moto uliozuka baada ya kushambuliwa na droni kutokea Iran.

Kiashiria cha Nikkei cha Tokyo kilipoteza zaidi ya 5% katika biashara ya mapema na bado kilikuwa kimeshuka kwa 4.57% karibu saa 9:10 usiku. Huko Seoul, kiashiria cha Kospi kilishuka kwa 3.13% kwani hakuna dalili za kupungua kwa uchumi zilizoonekana katika Mashariki ya Kati, ambapo vita vimeingia mwezi wake wa pili.

Kiashiria cha S&P 500 huko Sydney kilishuka kwa 0.9%, Taipei kilishuka kwa 2.14%, huku kiashiria cha Hang Seng cha Hong Kong kikipoteza 1.55%.

Vita katika Mashariki ya Kati vimeongezeka kutokana na kuingia kwa waasi wa Houthi katika mzozo huo. Wawekezaji wanazidi kuwa na wasiwasi kuhusu uwezekano wa Marekani kutuma wanajeshi wa ardhini.

Spika wa bunge la Iran Mohammad Bagher Ghalibaf aliishutumu Marekani siku ya Jumapili kwa kuandaa mashambulizi ya ardhini hata kama inatetea kujadili makubaliano, kufuatia kuwasili kwa meli ya kivita ya Marekani iliyokuwa na wanajeshi wapatao 3,500 Mashariki ya Kati. Matamshi yake yalikuja wakati mazungumzo yalipokuwa yakifanyika nchini Pakistan na Saudi Arabia, Uturuki, na Misri.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *