Watu 19 wamefariki dunia na wengine 58 kuokolewa baada ya boti ya wahamiaji kuharibika katika Bahari ya Mediterania ikitokea Libya kuelekea Ulaya.
Waliookolewa, wakiwemo watoto watano, walipelekwa katika kisiwa cha Lampedusa nchini Italia, huku watu watatu wakiripotiwa kupotea.
Kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji, IOM, wengi wa waliofariki walikufa kwa baridi kali baada ya kukaa baharini kwa siku kadhaa.
Takwimu zinaonyesha kuwa hadi sasa mwaka huu, zaidi ya watu 640 wamepoteza maisha katika njia ya kati ya Mediterania, ikiwa ni miongoni mwa viwango vya juu zaidi katika miaka ya hivi karibuni.
#kilichoborakabisa

(Feed generated with FetchRSS)