• Wachezaji wa Iran walilazimishwa kuondoka Marekani mara moja baada ya mechi yao ya kwanza ya Kombe la Dunia 2026 dhidi ya New Zealand
  • Iran, ambao wamekuwa na mvutano wa kisiasa na Marekani ya Donald Trump kwa muda sasa, wanakaa Tijuana, Mexico
  • Kocha mkuu Amir Ghalenoei alikosoa vikali uamuzi huo huku timu ikiendelea kukumbana na vikwazo katika kampeni yao ya Kombe la Dunia

Iran walilazimishwa kuondoka Marekani mara moja baada ya kumalizika kwa mechi yao dhidi ya New Zealand Jumatatu asubuhi.

Mehdi Taremi anaongoza Iran kabla ya mchezo wao wa Kombe la Dunia 2026 dhidi ya New Zealand, je Marekani na Iran bado wako vitani?
Mehdi Taremi anaongoza Iran kabla ya mchezo wao wa Kombe la Dunia 2026 dhidi ya New Zealand. Picha na Tayfun Coskun.
Source: Getty Images

Iran walifungua kampeni yao ya Kombe la Dunia 2026 kwa sare dhidi ya New Zealand katika Uwanja wa SoFi uliopo Los Angeles.

Team Melli walilazimika kusawazisha mara mbili na kuokoa pointi baada ya Chris Wood na Elijah Just kutishia kushinda mchezo huo kwa New Zealand. Mshambuliaji wa Nottingham Forest alimtengenezea Just mara mbili kufunga mabao mawili yasiyotarajiwa.

Hata hivyo, Iran, ambao wapo nafasi ya 20 duniani, walijibu kupitia Ramin Rezaeian na Mohammad Mohebi kuhakikisha timu zote mbili zinatoka na pointi moja.

Pia soma

Magazeti ya Kenya, Juni 16: Ndani ya dili ya KSh 375b iliyopewa tajiri wa Zimbabwe kuboresha JKIA

Iran walilazimishwa kuondoka Marekani baada ya mechi ya Kombe la Dunia 2026

Nchi hiyo ya Ghuba ilitarajia kufanya mazoezi ya kupona (recovery sessions) Los Angeles kabla ya kurudi katika kambi yao Mexico siku iliyofuata, lakini walilazimishwa kuondoka Marekani mara moja.

“Baada ya mchezo wa leo walituambia, ‘Lazima muondoke mara moja. Ilhali leo ni muhimu sana kwetu kufanya recovery. Tumeombwa kupanda ndege na kurudi kambini Tijuana, na tumekasirishwa sana na hilo. Wanatulazimisha kurudi mapema. Wanaifanya hali kuwa ngumu zaidi na zaidi, vikwazo zaidi, lakini hatutakubali hilo lituzuie kufanya vizuri,” alisema kocha mkuu Amir Ghalenoei.

Iran wamekumbana na vikwazo vingi kushiriki mashindano ya mwaka huu kutokana na mvutano wa kisiasa kati ya serikali yao na Marekani.

Iran head coach Amir Ghalenoei, World Cup 2026: Iran Forced To Leave USA Immediately After New Zealand Draw, What did Donald Trump say about Iran? Iran's matches at World Cup 2026
Kocha mkuu wa Iran Amir Ghalenoei (mwenye nguo nyeusi). Picha na Richard Heathcote.
Source: Getty Images

Wakati fulani, walifikiria kujitoa kabisa baada ya kukumbana na matatizo ya visa. Marekani ilikataa kuwahudumia ndani ya nchi hiyo, na kulazimisha timu hiyo kuhamia Mexico. FIFA pia ilikataa kuhamisha mechi zao za kundi kwenda Mexico.

Je, Iran na Marekani bado wako vitani?

Hii inakuja wakati Rais wa Marekani Donald Trump alipotangaza makubaliano ya amani yakimaliza vita vinavyoendelea kati ya nchi hizo mbili.

Pia soma

Magazetini: Ushindi Mkubwa kwa Sifuna! baada ya Gavana Kang’ata Kujiunga na Linda Mwananchi

Walikubaliana kusitisha mapigano kwa siku 60, hatua itakayofungua tena Mlango muhimu wa Hormuz.

Nini kinafuata kwa Iran katika Kombe la Dunia 2026?

Ikiwa na pointi moja na bado ikiwa na mechi mbili zilizosalia, Iran bado iko katika nafasi ya kufuzu hatua ya mtoano. Watarudi Los Angeles kucheza dhidi ya Ubelgiji tarehe 21 Juni kabla ya kumaliza kampeni yao dhidi ya Misri ya Mohamed Salah tarehe 27 Juni huko Seattle.

Ubelgiji na Misri zilicheza sare ya 1-1, ikimaanisha kila timu iko sawa kwa pointi katika Kundi G.

Donald Trump kuvunja kanuni za FIFA

Wakati huo huo, Donald Trump ataruhusiwa kuvunja kanuni za FIFA wakati wa mechi ya mwisho.

Trump alikosa hafla ya ufunguzi lakini atakuwepo kwa mechi ya mwisho tarehe 19 Julai.

Rais huyo wa Marekani alihusika katika tukio tata mwaka jana wakati wa Kombe la Dunia la Klabu.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *