
Marekani imekiwekea vikwazo kiwanda cha kusafisha madini cha Rwanda kwa biashara haramu ya dhahabu inayohusishwa na waasi nchini DRC.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Marekani imewawekea vikwazo watu wawili na makampuni manne ya madini ya Rwanda, ikiwashutumu kwa kuendesha mtandao wa magendo ya madini kwa manufaa ya M23, kundi la waasi wenye silaha linaloendesha harakati zake nchini jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Tangu kuibuka tena mwaka wa 2021, M23 imedhibiti maeneo makubwa ya mashariki mwa DRC, eneo lenye utajiri wa dhahabu, bati, na koltani, madini muhimu kwa utengenezaji wa bidhaa za kielektroniki.
Marekani inawatuhumu kwa kuendesha biashara ya magendo ya madini inayowanufaisha waasi wa kundi la M23 katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Wizara ya Fedha ya Marekani imesema vikwazo hivyo vipya vinalenga Kiwanda cha Kuchakata Dhahabu cha Gasabo, ambacho Washington ilisema “kilikuwa kama mshirika muhimu wa maafisa wa serikali ya Rwanda na waasi wa M23 walipokuwa wakitafuta na kusafirisha dhahabu kutoka mashariki mwa Kongo.”
Ilisema dhahabu ilisafirishwa kutoka mashariki mwa Kongo na M23 na Vikosi vya Ulinzi vya Rwanda (RDF) hadiRwanda, na kisha ikahamishwa kupitia usafiri wa ardhini na angani hadi kiwanda cha kuchakata cha Gasabo jijini Kigali. Ilisema angalau kilo 60 za dhahabu — zenye thamani ya mamilioni ya dola za Marekani — zilisafirishwa kutoka mashariki mwa DRC hadi Gasabo Gold kupitia mfumo huu mapema mwaka 2026. Vikwazo hivyo vipya viliwalenga Mwenyekiti wa Gasabo Gold, Jean Malic Kalima na Meneja Mkuu Bosco Kayobotsi. Pia vililenga makampuni mengine matatu ya madini yanayodaiwa kuwa na uhusiano na Kalima.
Hii inaimarisha kujitolea kwa Marekani kutekeleza mfumo wa ujumuishaji wa uchumi wa kikanda unaolenga kupanua biashara na uwekezaji, kuongeza uwazi katika minyororo muhimu ya usambazaji wa madini, na kuweka msingi wa mtazamo bora wa kiuchumi wa muda mrefu kwa eneo lote, kulingana na taarifa iliyotolewa na serikali ya Marekani.
“Marekani haitaruhusu makundi ya wahalifu kunufaika kutokana na biashara haramu ya madini na kuvuruga usalama wa eneo hilo,” alisema Waziri wa Fedha Scott Bessent. “Utajiri wa madini ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni haki kwa raia wa Kongo. Chini ya uongozi wa Rais Trump, tutaendelea kuchukua hatua kali dhidi ya wale wanaowezesha vurugu, uchimbaji haramu, na mashambulizi dhidi ya raia wa Kongo.”