- Seneta Edwin Sifuna alipinga matarajio ya mbunge Didmus Barasa ya kuwania ugavana katika mazishi, akishutumu mbinu zake za kisiasa
- Barasa alitetea kutoa misaada kwa wakazi na kuwashutumu baadhi ya viongozi wa Linda Mwananchi kwa uchoyo na ufujaji
- Harakati za Linda Mwananchi zilishika kasi huku Sifuna akilenga kuwaunganisha viongozi wa upinzani kwa ajili ya mabadiliko
Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna ametangaza mkutano mkubwa mjini Bungoma kuelezea mwelekeo wa Linda Mwananchi kabla ya uchaguzi wa 2027.

Source: Facebook
Sifuna alizungumza Jumamosi, Julai 4, wakati wa mazishi ya kaka yake Mbunge Jack Wamboka, Eric Wamboka, huko Siboti, Jimbo la Bumula.
Sifuna alimwambia nini Didmus Barasa?
Katika mazishi hayo, Sifuna alisema Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa hawezi kujiunga na timu yake. Pia aliwahurumia wakazi wa Bungoma wanaomuunga mkono Barasa kuwa gavana mwaka wa 2027.
“Kuna sababu tunazosema Ruto lazima aondoke. Anawazalisha waathiriwa wa vurugu za polisi zaidi ya vile anavyoweza kuwalipa. Nimechoka kama kiongozi wa upinzani. Kila siku unaamka na visa vya madaktari, walimu, na Ebola. Hata kama upinzani unakusudiwa kuizuia serikali, huu unatupa kazi ngumu,” alisema, akiwahimiza Barasa na Mbunge John Waluke kumshawishi rais ili upinzani uweze “kupumzika kwa wiki mbili” bila madai ya ukandamizaji.

Pia soma
Linda Mwananchi wathibitisha Gachagua hawamuachi kamwe, wasema kumng’oa Ruto ni juhudi ya kila mtu
Sifuna alipinga azma ya Barasa ya kuwa gavana, akimtuhumu kwa kushindwa kuwatetea wenyeji wakati wa uuzaji wa Kampuni ya Sukari ya Nzoia. Pia alidai Barasa anatumia pesa kupata uungwaji mkono.
“Barasa, huwezi kwenda bungeni na kupitisha muswada unaowakandamiza Wakenya, kisha Ijumaa, unatembea hadi Tawi la KCB Bungoma, unapoteza noti za KSh 100, na kuzisambaza kwa watu. Kisha unaendelea na kuchapisha kwenye mtandao kwamba watu hawamtaki Sifuna. Tumekujua, na kwa sababu hiyo, utakuwa mtu wa mwisho kuondoka kwenye mazishi haya,” alisema.
Wakati huo huo, Barasa alikana kutoa misaada, akisema matendo yake yanaonyesha ukarimu. Aliwashutumu baadhi ya viongozi wa Linda Mwananchi kwa uchoyo.
Hotuba yake ilikatizwa baada ya kukejeli alipomkosoa seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi, akimtuhumu kwa kutumia fursa.
“Kama kuna mtu katika timu hii ambaye ninamheshimu sana kwa akili yake, ni Osotsi… Yuko katika timu ya Sifuna kuhesabu nafasi na faida zake, si kwamba anampenda… Kila mtu ana haki ya kuzungumza, na ikiwa unakuja kunishinda, basi niache niachie kipaza sauti niondoke,” Barasa alisema kabla ya kuondoka.

Source: Facebook
Lini Linda Mwananchi watafanya mkutano Bungoma?
Seneta huyo mchapakazi alshukuru uungaji mkono kwa Linda Mwananchi kutoka eneo la Mahgharibi, kundi ambalo limepata umaarufu kote nchini.

Pia soma
Picha: Wetang’ula, Ichung’wah wapokea makaribisho ya kishujaa Eldoret katika mkutano wa UDA
Aliwasihi viongozi wengine wa upinzani kuwashawishi wapiga kura kuunga mkono mawazo mbadala ya kundi lake hilo ili kubadilisha nchi.
Sifuna alisema kwamba timu ya Linda Mwananchi itaandaa mkutano mkubwa huko Bungoma mnamo Julai, ukiwajumuisha makasisi, vijana, wanawake, na viongozi wa walimu.
“Tutaandaa mkutano mkubwa hapa Bungoma. Utakachoniambia niseme, nitafanya Nairobi. Nataka tu uwe na subira kwa sababu hii ni nafasi ya maisha na tuna jukumu la kujibu wito wa kizazi chetu,” alisema.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke