• Zambia inaomboleza kifo cha aliyekuwa Makamu wa Rais, Dkt. Guy Lindsay Scott, aliyehudumu chini ya marehemu Rais Michael Sata na kwa muda mfupi kuwa kaimu mkuu wa nchi
  • Serikali imethibitisha kuwa alifariki baada ya kuugua kwa muda mfupi na kutangaza kuwa Rais Hakainde Hichilema amemuidhinishia mazishi ya kitaifa kwa kutambua mchango wake kwa taifa
  • Wananchi watajulishwa ratiba ya mazishi mara tu mpango wa mazishi utakapokamilika

Zambia imepoteza mmoja wa wanasiasa wake mashuhuri kufuatia kifo cha aliyekuwa Makamu wa Rais, Dkt. Guy Lindsay Scott.

Makamu wa Rais wa zamani wa Zambia Dkt Guy Lindsay Scott
Makamu wa rais wa zamani wa Zambia Guy Scott amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 82. Picha: Zambia Daily.
Source: UGC

Katika taarifa iliyotolewa Jumatano, Julai 15, serikali ya Zambia ilitangaza kuwa Scott alifariki mapema siku hiyo katika shamba lake la Trotover Farm, eneo la Leopards Hill, Lusaka, baada ya kuugua kwa muda mfupi. Alikuwa na umri wa miaka 82.

“Serikali ya Jamhuri ya Zambia inasikitika kuwafahamisha wananchi kuhusu kifo cha Mheshimiwa Dkt. Guy Lindsay Scott, aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Zambia,” taarifa hiyo ilisema.

Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Zambia alifariki vipi?

Pia soma

Magazetini: Vurugu zatikisa mikutano ya Linda Mwananchi, wahuni wavamia Kisumu na Nyahururu

Kwa mujibu wa serikali, Scott alifariki Jumatano, Julai 15, katika shamba lake lililoko Leopards Hill.

Scott alihudumu kama Makamu wa Rais wa Zambia kuanzia mwaka 2011 hadi 2014 chini ya rais wa tano wa nchi hiyo, marehemu Michael Chilufya Sata.

Baada ya kifo cha Sata mnamo Oktoba 28, 2014, Scott alichukua nafasi ya kaimu rais, akiiongoza Zambia kuanzia Oktoba 2014 hadi Januari 2015 wakati nchi ilipokuwa ikijiandaa kwa uchaguzi wa urais.

Kabla ya kuwa Makamu wa Rais, Scott pia aliwahi kuhudumu kama Waziri wa Kilimo, Chakula na Uvuvi katika serikali ya aliyekuwa Rais Frederick Chiluba.

Serikali ya Zambia ilimwelezea Scott kama mtumishi wa umma aliyekuwa mashuhuri, ambaye mchango wake katika maendeleo ya kisiasa na ya taifa utakumbukwa kwa muda mrefu.

Aliyekuwa makamu wa rais wa Zambia Guy Scott afariki dunia
Makamu wa rais wa zamani wa Zambia Guy Scott afariki dunia akiwa na umri wa miaka 82. Picha: History’s Shadow.
Source: UGC

Guy Scott atazikwa kwa mazishi ya kitaifa

Rais Hakainde Hichilema ameagiza kuwa Scott apewe mazishi ya kitaifa kwa heshima ya huduma yake kwa taifa.

“Rais wa Jamhuri ya Zambia, Bw. Hakainde Hichilema, ameidhinisha aliyekuwa Makamu wa Rais kupewa mazishi ya kitaifa kwa kutambua mchango wake mkubwa wa kitaaluma na kisiasa kwa taifa,” taarifa hiyo ilisema.

Pia soma

Abubakar Zein: Aliyekuwa mbunge wa EALA azikwa katika makaburi ya Lang’ata saa chache baada ya kifo

Serikali iliongeza kuwa wananchi watajulishwa ratiba ya mazishi mara tu mpango wa mazishi utakapokamilika.

“Wananchi wanaarifiwa kuwa ratiba ya mazishi ya kitaifa itatangazwa kwa wakati unaofaa.”

Taarifa hiyo ilisainiwa na Katibu wa Baraza la Mawaziri, Patrick K. Kangwa.

Scott aliingia kwenye historia kama kiongozi wa kwanza mweupe wa nchi barani Afrika katika kipindi cha miaka 20, baada ya aliyekuwa rais, “King Cobra” Michael Sata, kufariki katika hospitali moja jijini London akiwa na umri wa miaka 77.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *