Kwa usiku wa saba mfululizo, Marekani imeishambulia Iran kwa mabomu siku ya Jumamosi, Julai 18. Tehran imelipiza kisasi kwa kushambulia maeneo ya Jordan, Kuwait, na Bahrain, huku ikitishia kuanzisha “shambulio kamili.” Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) ilmesema ilishambulia “maeneo ya uangalizi, miundombinu ya vifaa vya kijeshi, maghala ya silaha za chini ya ardhi, na mali za baharini” nchini Iran.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Katika siku ya saba ya mashambulizi yake dhidi ya Iran, Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM) iliripoti kwamba ilishambulia “maeneo ya uangalizi, miundombinu ya vifaa vya kijeshi, maghala ya silaha za chini ya ardhi, na mali za baharini,” bila kutaja malengo yoyote ya raia, usiku wa Ijumaa kuamkia Jumamosi.

Mamlaka katika jimbo la Hormozgan kusini mwa Iran imetangaza kwamba mashambulizi ya anga ya Marekani katika jimbo hilo yamewaua watu wasiopungua watatu na kuwajeruhi wanane, yakilenga madaraja mawili na barabara za chini ya ardhi, kulingana na shirika la habari la serikali la IRNA. Jamhuri ya Kiislamu imerudia tishio lake la kulipiza kisasi kwa kushambulia “miundombinu yote katika eneo la Ghuba” ikiwa “Marekani itashambulia miundombinu ya Jamhuri ya Kiislamu.”

Tehran ilitangaza siku ya Ijumaa, Julai 17, kwamba ilizindua mashambulizi mapya katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na kituo cha amri cha Marekani huko Al-Tanf, Syria. Hii inakuja baada ya kulenga vituo vya kijeshi vya Marekani huko Jordan kwa kutumia ndege zisizo na rubani mnamo Julai 16, kulingana na televisheni ya serikali, kufuatia mashambulizi zaidi ya anga ya Marekani nchini Iran. Tehran pia ilidai kushambulia vituo vya Marekani huko Bahrain na Kuwait mapema Ijumaa asubuhi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *