Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alianza safari yake ya kwanza rasmi barani Afrika mnamo Novemba 20, akitua Mauritius, nchi inayochukuliwa kuwa “jirani wa kimkakati” wa Ufaransa kutokana na ukaribu wake wa kijiografia na Kisiwa cha Réunion. Rais wa Ufaransa na waziri mkuu wa Mauritius wametoa taarifa ya pamoja Alhamisi jioni huko Port Louis. Wawili hao wameonyesha nia yao ya pamoja ya kufufua uhusiano kati ya Ufaransa na Mauritius.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Hili lilikuwa lengo la awamu hii ya kwanza ya ziara ya Emmanuel Macron barani Afrika: “kufufua uhusiano” na Mauritius, ambapo hakuna rais wa Ufaransa aliyefanya ziara rasmi kwa zaidi ya miaka thelathini.

Waziri Mkuu wa Mauritius Navin Ramgoolam amezungumzia “uhusiano wa kihistoria na wa kirafiki” unaounganisha nchi yake na Ufaransa, huku Emmanuel Macron akithibitisha “kujitolea pakubwa kwa Bahari ya Hindi” na “maono ya pamoja ya changamoto kuu” zinazoikabili Ufaransa kwa sasa.

Waawili hao wamejadili “masuala kadhaa makubwa,” ikiwa ni pamoja na ushirikiano wa vyuo vikuu, nishati na usambazaji wa maji, na masuala ya usalama, miongoni mwa mengine.

Mzozo kati ya nchi hizo mbili kuhusu uhuru wa Kisiwa cha Tromelin, mojawapo ya Visiwa vilivyotawanyika, pia umejadiliwa. Mjadala ulikuwa “mzuri na wa wazi,” kulingana na Waziri Mkuu Navin Ramgoolam, na Emmanuel Macron amesema kwamba “suala hili halipaswi kusababisha mgawanyiko.”

Hatimaye, viongozi hao wawili walijadili hali nchini Madagascar. Kwa mara ya kwanza, Emmanuel Macron alithibitisha kwamba “Ufaransa itaunga mkono (mpito nchini Madagascar) kwa mtazamo wa wazi” na “kuweka kipaumbele katika usaidizi kwa raia wa Madagascar, haswa kuhusu maendeleo ya kiuchumi, vijana, na mapambano dhidi ya ufisadi na utajiri haramu.”

“Tulithibitisha tena malengo yetu ya pamoja, haswa kuhusu Madagascar, nchi rafiki inayopitia mabadiliko makubwa. Tulitambua kujitolea kwa mamlaka mpya kushughulikia matarajio ya vijana”, amesema rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu Ramgoolam amesema “anaunga mkono kikamilifu juhudi za Ufaransa na mbinu ya Umoja wa Ulaya, Umoja wa Afrika, na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ya kuleta utulivu haraka iwezekanavyo” kisiwani humo.

Rais Macron anaedelea na ziara nchini Mauritius 

Rais wa Ufaransa anaendelea na ziara yake nchini Maurituis leo Ijumaa, Novemba 21. Ahadi za Emmanuel Macron zinaendelea, kwanza nchini Mauritius Ijumaa hii asubuhi. Rais wa Ufaransa atapanda meli ya Ufaransa Champlain.

Meli hii ya Jeshi la Wanamaji la Ufaransa inashiriki katika misheni za pamoja za ufuatiliaji wa baharini na walinzi wa pwani wa Mauritius na inachangia ushirikiano wa kikanda kuhusu usalama wa baharini. Mapambano dhidi ya biashara haramu ya binadamu na uvuvi haramu ni miongoni mwa mada zilizojadiliwa wakati wa mkutano kati ya Emmanuel Macron na Waziri Mkuu wa Mauritius Navin Ramgoolam.

Ijumaa asubuhi, rais wa Ufaransa atazindua ubalozi mpya wa Ufaransa nchini Mauritius kabla ya kuelekea nchni Afrika Kusini kwa mfululizo wa mazungumzo ya pande mbili kabla ya mkutano wa kilele wa G20. Emmanuel Macron anatarajiwa kukutana kwa muda mfupi na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, ikifuatiwa na sherehe ya kumbukumbu ya kuwaenzi Wafaransa waliopigana dhidi ya ubaguzi wa rangi.

Jioni, rais atashiriki katika uzinduzi wa Baraza la Biashara la Ufaransa na Afrika Kusini ili kuwezesha na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya makampuni katika nchi zote mbili, unaotokana na ushirikiano uliopo kati ya Ufaransa na Nigeria.

Hatua za mwisho

Kisha, Emmanuel Macron atasafiri hadi Gabon “kuthibitisha na kuimarisha” ushirikiano ulioelezewa na Ikulu ya Élysée kama wenye “ubora, ulioboreshwa, na unaosonga mbele.” Hii itakuwa ziara ya kwanza ya kiserikali ya rais wa Ufaransa huko Libreville tangu Brice Oligui Nguema aingie madarakani.

Hatimaye, ziara ya rais barani Afrika itakamilika mapema wiki ijayo huko Luanda, Angola, pamoja na mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika. Lengo la mkutano huo litakuwa, haswa, kutathmini maendeleo yaliyopatikana tangu mkutano wa mwisho wa pamoja, ambao ulifanyika Brussels mnamo 2022, wakati Ufaransa ilipokuwa mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Ulaya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *