Hatua za kuendeleza mradi huo zilianza mwishoni mwa miaka ya 1990 wakati Rio Tinto, kampuni ya uchimbaji madini ya Anglo-Australia, ilipogunduwa kwa mara ya kwanza kiwango kikubwa kinachoweza kutumika kwa biashara katika milima ya Simandou. 

Tangu wakati huo, hatua zimekwamishwa kutokana na hali mbaya ya usalama na kubadilika kwa mamlaka kila mara.

Ukiwa na thamani ya zaidi ya dola bilioni 23, mradi wa Simandou ndio ubia mkubwa zaidi wa madini kuwahi kufanyika.

Unajumuisha ujenzi wa reli ya kilomita 552 inayounganisha migodi miwili mipya katika Milima ya Simandou na bandari mpya ya kina kirefu kwenye pwani ya Guinea.

Uzalishaji unatarajiwa kuongeza hadi tani milioni 120 za madini ya chuma ya kiwango cha juu kila mwaka ifikapo 2030, kiwango ambacho kitasawazisha usambazaji kimataifa kwa kiasi kikubwa.

Robo tatu ya mapato yake yataelekea China ambapo kwa sasa inamiliki asilimia 75 ya mradi wa uchimbaji madini. Serikali ya Guinea tapata 15% ya jumla ya mapato kutoka kwa kila moja ya migodi miwili  ya uchimbaji vya madini.

Ingawa kwa sasa Guinea si miongoni mwa wazalishaji wakuu wa madini ya chuma duniani, inatarajiwa kupanda hadi nafasi ya tatu punde tu migodi ya Simandou itakapofikia uwezo wake kamili nchini humo ambapo uchimbaji madini kwa sasa unachangia karibu 2.2% ya mapato ya Taifa.

Makadirio ya serikali ya Guinea yanaonyesha mradi huu wa madini ya chuma pekee unaweza kuongezea serikali mapato hadi kufikia dola bilioni 1 kila mwaka iwapo itazalisha kikamilifu kwa ajili ya biashara duniani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *