
Waziri Mkuu wa Italia Giorgia Meloni anajiandaa kutetea maslahi ya Italia—nchi ya kwanza ya Magharibi kutambua uhuru wa Angola mnamo Februari 1976—wakati wa mkutano wa kilele wa Luanda kati ya Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika, unaofanyika Novemba 24 na 25. Atazungumzia vyema Mpango wa Mattei kwa Afrika, uliowasilishwa rasmi mwaka wa 2024, kwa ufadhili wa awali wa takriban euro Bilioni 5.5, kulingana na serikali ya Italia.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Roma, Anne Le Nir
Kwa ujumla, Mpango wa Mattei unalenga kuimarisha uhusiano kati ya Italia na Afrika kupitia ushirikiano wa usawa katika njanja kama vile nishati, afya, kilimo, na miundombinu. Msingi wa hili ni lengo la kuzuia wimbi la wahamiaji. Giorgia Meloni anauita “haki ya kutohama.”
Mpango huu, unaohusu nchi 14 za Afrika, unatarajiwa kuwa mada kuu katika mkutano wa kilele wa Luanda, hasa kwa kuwa Angola imejumuishwa kwa miezi kadhaa. Kwa sasa, uhusiano wake na Italia kimsingi ni wa kiuchumi.
Angola ni miongoni mwa wauzaji kumi bora wa mafuta kwa Italia na pia huipa gesi asilia iliyoyeyushwa. Italia, kwa upande wake, husafirisha nje zana za mashine na bidhaa za kilimo.
Kwa Roma, ambayo mpango wake wa Mattei unaendana na mkakati wa Ulaya wa Global Gateway, suala lingine muhimu, kwa upande wa maslahi ya kiuchumi na kijiografia, litakuwa Lobito Corridor. Mradi huu wa reli na miundombinu unakusudiwa kuunganisha Angola na maeneo ya madini ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Zambia.