Malawi imeidhinisha matumizi ya sindano za kufubaza VVU ijulikanayo kama lenacapavir, na kuwa taifa la nne barani Afrika kupitisha dawa hiyo.

Dawa hiyo iliyotengenezwa na kiwanda cha Gilead Sciences Ireland, UC, hutolewa kupitia sindano, kila baada ya miezi sita.

Mamlaka ya Udhibiti Madawa na Famasia nchini Malawi (PMRA) ilipitisha dawa hiyo kufuatia siku 46 za majaribio.

Kulingana na Dkt. Beatrice Matanje, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Ukimwi nchini humo (NAC), amepongeza hatua hiyo, akiiita ni ya muhimu ya kupambana na VVU nchini humo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *