[ad_1]

Maelezo ya video, CCTV yanawa wakati Israel ilipowashambulia viongozi wa Hamas mjini Doha

    • Author, Jeremy Bowen
    • Nafasi, Mhariri wa Kimataifa

Takriban mwaka mmoja uliyopita nilimhoji kiongozi wa Hamas na mpatanishi mkuu Khalil al-Hayya in Doha. Nilikutana naye katika nyumba moja ambayo haikuwa mbali na jengo ambalo lilishambuliwa na Israel siku ya Jumanne.

Tangu vita vya Gaza vilipozuka, al-Hayya amekuwa mpatanishi mkuu wa Hamas, akituma na kupokea ujumbe kwa Waisraeli na Wamarekani kupitia wapatanishi wa Qatar na Misri.

Wakati ambapo kulikuwa na matumaini ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitishaji mapigano, al-Hayya, pamoja na wanaume ambao pia walilengwa hiyo jana, walikuwa umbali mfupi tu kutoka kwa wajumbe wa Israeli na Marekani.

Waliposhambuliwa, al-Hayya na viongozi wengine wakuu wa Hamas walikuwa wakijadili mapendekezo ya hivi punde ya kidiplomasia ya Marekani ya kumaliza vita huko Gaza na kuwaachia huru mateka wa Israel waliosalia.

[ad_2]

Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *