
Akizunguma katika hotuba ya kuashiria kuanza kwa Cyprus kushika urais wa kupokezana wa Umoja wa Ulaya amesema hakuna kitu kinachoweza kuamuliwa kuhusu Greenland bila Denmark. Na kuongeza kuwa watu wa eneo hilo “Wana uungwaji mkono kamili na mshikamano wa Umoja wa Ulaya.” Katika siku za hivi karibuni Rais Donald Trump wa Marekani, Donald Trump, amekuwa akirejea kauli ya kwamba anataka kuichukua Greenland, akidai kisiwa hicho ni muhimu kwa mkakati wa kijeshi wa Marekani na akisema Denmark haijafanya vya kutosha kukilinda.