Gavana wa California kutoka chama cha Democratic, Gavin Newsom, amewasihi viongozi wa nchi za Ulaya huko Davos, Uswizi, siku ya Jumanne “kusimama” dhidi ya Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu suala la Greenland, hata kufikia hatua ya “kumpiga usoni” ili kumfanya asitishe hatua zake mbovu.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Katika hotuba yake katika Jukwaa la Uchumi Duniani, Bw. Newsom alimwita Trump “dhaifu” na akasema Umoja wa Ulaya (EU) lazima “umjibu kwa nguvu kubwa”.

“Yeye ni mtaalamu wa kutumia udhaifu, lakini anasiisha hatua zake unapompiga usoni,” amesema. “Huwezi kuweka pamoja mbuzi na Karoti. adabu inatosha,” ameongeza. “Acheni kujaribu kumtuliza. Pambaneni jino kwa jino, moto kwa moto.” Bw. Newsom ameita tamaa ya rais wa Marekani ya kutaka kuiteka Greenland kuwa ya “wendawazimu,” lakini akasisitiza kwamba Bw. Trump hatajaribu kushinda “kijeshi” kisiwa hicho cha Denmark kinachojitawala. “Jambo hili lote la Greenland ni la kipuuzi, na ni wakati wa kila mtu kutambua hali hiyo, kusimama imara na kuazimia, kujitetea, na kuzungumza kwa sauti moja. Mpigeni usoni,” Bw. Newsom amesema.

Bunge la Ulaya lasitisha uidhiniswaji wa makubaliano ya biashara na Marekani

Bunge la Ulaya limeamua kusitisha mchakato wa kuidhinishwa kwa makubaliano ya biashara kati ya Umoja wa Ulaya na Marekani, kufuatia vitisho vya hivi karibuni kutoka kwa Donald Trump, makundi yake makuu ya kisiasa yamebiisha siku ya Jumanne. Kuna “makubaliano mengi” miongoni mwa makundi ya kisiasa ya kusitiisha makubaliano ya biashara yaliyohitimishwa mwaka jana kati ya Marekani na EU, kiongozi wa kundi la S&D, Iratxe Garcia Perez, amewaambia waandishi wa habari.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *