Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, siku moja baada ya Baraza la Katiba kutangaza matokeo ya mwisho ya uchaguzi wa urais, na kumthibitisha Faustin-Archange Touadéra kuwa mkuu wa Jamhuri ya Saba kwa asilimia 77.90 ya kura, Anicet-Georges Dologuélé ameamua kuvunja ukimya wake. Alishika nafasi ya pili katika uchaguzi wa urais kwa asilimia 13.5 ya kura. Alizungumza siku ya Jumanne, Januari 21, huko Bangui wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Anicet-Georges Dologuélé ameishutumu Mamlaka ya Kitaifa ya Uchaguzi na Baraza la Katiba kwa kushindwa kwa majukumu yao, akitaja uchaguzi uliogubikwa na udanganyifu mkubwa, ambao aliona hauaminiki wala haueleweki. Kulingana naye, serikali ya sasa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati imetekeleza mifumo inayolenga kuzuia mchakato wa kidemokrasia na kudhoofisha utawala wa sheria. Licha ya shutuma hizi, kiongozi huyo wa upinzani anawataka watu wasikate tamaa, akidai kwamba ukweli hatimaye utajulikana.

“Udanganyifu mkubwa”

“Baraza la Katiba limechagua kuunga mkono uchaguzi uliogubika udanganyifu mkubwa na kasoro kubwa,” Anicet-Georges Dologuelé alimwambia Rolf Steve Domia-leu, mwandishi wetu huko Bangui. “Baraza la Katiba limechagua kupuuza ombi letu la kufuta uchaguzi huu, ambao hata hivyo kuna ushahidi wa kutosha. Lilichukuwa uamuzi wa kushangaza wa kuongeza idadi ya wapiga kura, ambao uliongezeka kutoka 52.42% hadi 64.42%, tofauti ya pointi kumi na mbili.”

“Uamuzi huu haufuti matokeo, wala ukweli, wala historia,” kiongozi huyo wa upinzani aliongeza. “Wakati uchaguzi unapofanyika kwa njia ya isiyosahihi, wakati mamlaka ya kitaifa ya uchaguzi inasaliti jukumu lake, wakati matakwa ya umma yanapotoshwa, si demokrasia inayoshinda, bali ni nguvu inayoponda sheria. Kwa wale wanaofikiri wameshinda kupitia udanganyifu na kejeli, nasema hivi: unaweza kushinda hukumu, lakini ukawapoteza raia”.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *