
Matarajio ni kwamba mataifa yatawasilisha michango mipya ya kitaifa (NDCs) pamoja na kuendeleza ahadi zilizotolewa wakati wa COP29 mwaka uliopita. Mkutano huo pia unatarajiwa kutafuta mbinu bunifu za ufadhili ili kusaidia nchi zinazoathirika zaidi na janga la tabianchi.
Katika hafla ya ufunguzi, Simon Stiell ambaye ni Katibu Mtendaji wa UNFCCC amesema matarajio ya miaka 10 iliyopita huko Paris ya kupunguza utoaji wa hewa chafuzi si haba yanaonekana lakini bado kuna changamoto ya kuhakikisha ongezeko la joto halivuki kiwango cha nyuzijoto 1.5 katika kipimo cha Selsiyasi.
Huu si wakati wa kulalamika bali kuchukua hatua
Hata hivyo amesema huu si wakati wa kulalamika bali ni wakati wa kusaka majawabu. “Tumekuja hapa Belém kwenye mdomo wa mto Amazon. Na tunaweza kujifunza mengi kutoka mto huu mkuu. Amazon si kitu kimoja pekee, bali ni mfumo mkubwa wa mito unaoungwa mkono na zaidi ya vijito 1,000. Ili kuharakisha utekelezaji, mchakato wa COP lazima uungwe mkono kwa njia hiyo – ukiendeshwa na mikondo mingi ya ushirikiano wa kimataifa –kwa sababu ahadi za kitaifa pekee hazipunguzi utoaji wa hewa chafuzi kwa kasi ya kutosha.”
Changamoto ni kubwa, chaguo li wazi – Guterres
Kila taifa lina haki ya kulinda haki ya binadamu kwenye mazingira
Naye Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, amesisitiza kwamba COP30 inapaswa kuwa “mgeuko muhimu” katika kuhakikisha uwajibikaji wa mataifa kuhusu tabianchi na haki za binadamu.
Wakimbizi wa madhara ya mabadiliko ya tabianchi waongezeka
Mkutano huo wa wiki mbili mjini Belém ukiwa wa kwanza kuandaliwa na Brazil baada ya zaidi ya muongo mmoja unalenga kuimarisha juhudi za dunia kuelekea ustahimilivu wa tabianchi, usawa na maendeleo endelevu.