
Rais wa Marekani Donald Trump leo Jumatatu, Novemba 10, amewasamehe watu 77 waliohusika katika jaribio la kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa urais wa mwaka 2020, akiwemo wakili wake wa zamani na meya wa zamani wa Jiji la New York Rudy Giuliani, kulingana na Ed Martin, afisa mkuu anayehusika na kupanga misamaha ya rais.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Tangazo hili linamaliza dhuluma kubwa ya kitaifa iliyofanywa dhidi ya watu wa Marekani baada ya uchaguzi wa urais wa mwaka 2020 na linaendelea na mchakato wa maridhiano ya kitaifa,” unasema ujumbe ulioandikwa siku ya Ijumaa na kuchapishwa mtandaoni na Ed Martin kwenye mtandao wa kijamii wa X mapema Jumatatu asubuhi.
Miongoni mwa wale waliopokea msamaha wa rais ni Mark Meadows, Mkurugenzi wa zamani katika Ikulu ya White House mnamo 2020; John Eastman, wakili aliyependekeza mikakati ya kuzuia uthibitisho wa matokeo ya uchaguzi wa urais ambayo Donald Trump alipoteza kwa faida ya Joe Biden; na wanaharakati kadhaa wa chama cha Republican waliohusika katika jaribio la kubatilisha matokeo ya uchaguzi.
Msamaha huo unaelezewa kama “kamili, usio masharti,” taarifa hiyo inabainisha, huku ikibainisha kwamba “msamaha huo haumhusu rais wa Marekani.”