Kwa mujibu wa taarifa za awali, watu sita wameuawa mjini Kyiv, huku wengine wawili wakiripotiwa kuuawa katika mji wa Chornomorsk kusini mwa nchi.

Mashambulizi hayo pia yamesababisha majeruhi kwa raia, uharibifu wa makazi na miundombinu ya nishati, pamoja na uharibifu wa ubalozi wa Jamhuri ya Azerbaijan uliopo jijini Kyiv.

Mashambulizi hayo yanakiuka sheria za kimataifa

Katika taarifa iliyotolewa na msemaji wake,mjini New York Marekani  Katibu Mkuu amesisitiza kuwa mashambulizi dhidi ya raia na miundombinu ya kiraia yanakiuka sheria za kimataifa za kibinadamu.

Ni mambo yasiyokubalika, popote pale yanapotokea, na lazima yakome mara moja, imesema taarifa hiyo, ikisisitiza pia kwamba majengo ya kidiplomasia ni maeneo yanayopaswa kulindwa kisheria.

Katibu Mkuu amekumbusha kanuni ya kutovunjwa kwa ulinzi wa maeneo ya kidiplomasia, akieleza kuwa taarifa za uharibifu wa ubalozi wa Azerbaijan zinasikitisha.

Guterres amerudia wito wake wa muda mrefu wa kutaka kusitishwa kwa mapigano kikamilifu, mara moja na bila masharti yoyote.

Wazima moto wanafanya kazi katika vifusi vya jengo la makazi huko Kyiv lililoharibiwa katika mgomo wa kombora mnamo Agosti 28.

© UNICEF/Oleksii Filippov

Wazima moto wanafanya kazi katika vifusi vya jengo la makazi huko Kyiv lililoharibiwa katika mgomo wa kombora mnamo Agosti 28.

Usitishaji mapigano ni wa lazima

Amesema hatua hiyo ni muhimu ili kufungua njia ya amani ya haki, jumuishi na endelevu nchini Ukraine,” ambayo itaheshimu kikamilifu mamlaka, uhuru na mipaka ya Ukraine kama inavyotambulika kimataifa.

Katibu Mkuu amesisitiza kuwa suluhu yoyote ya mgogoro huo lazima izingatie Mkataba wa Umoja wa Mataifa, sheria za kimataifa, na maazimio husika ya Umoja wa Mataifa.

Wito huo mpya unatolewa wakati Ukraine ikikabiliwa na ongezeko la mashambulizi dhidi ya gridi ya nishati na miji yake kuelekea msimu wa baridi kali, hali inayoongeza hofu ya mateso zaidi kwa raia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *