
Akizungumza katika mkutano wa mataifa hayo mawili mjini Beijing Klingbeil amesema Ujerumani na China pamoja zinaweza kuwa na majibu ya changamoto zinazowakabili.
Waziri huyo wa fedha ndio muakilishi wa kwanza wa serikali ya muungano Ujerumani kuitembelea China huku Berlin ikipitia shinikizo la kuonyesha inaweza kushughulikia sera ya China huku kukiwa na pengo kubwa la kibiashara.
Makampuni ya Ujerumani yamechangia ukuaji na uwekezeaji katika sekta ya teknolojia na uhandisi, China.