
Trump aliandika kwenye Truth Social: “Hii itakuwa moja ya idhini kubwa zaidi katika historia ya Umoja wa Mataifa, itasababisha amani zaidi duniani, na ni tukio la kihistoria.” Azimio hilo lilipitishwa Jumatatu jioni kwa kura 13 za kuunga mkono, huku Urusi na China zikijizuia. Mpango huo unajumuisha kupeleka kikosi cha kimataifa kusaidia kudumisha usitishaji wa mapigano kati ya Israel na Hamas.Trump alisifu waliounga mkono pendekezo hilo lakini hakutaja Israel, Hamas au Wapalestina katika kauli yake. Azimio linategemea mpango wa vipengele 20 alioutangaza Septemba, unaopendekeza Gaza kusimamiwa kwa muda na kamati ya wataalamu wa Kipalestina wasioegemea upande wowote na wataalamu wa kimataifa, chini ya chombo kipya cha mpito kiitwacho Bodi ya Amani, ambacho Trump anasema atakiongoza.