Askofu Mkuu wa Bamenda nchini Cameroon, ametoa wito mwingine wa kukomesha mgogoro katika maeneo mawili yanayozungumza Kiingereza. Wiki iliyopita wa mapadri kadha walitekwa nyara  katika mkoa wa Kaskazini Magharibi. Katika taarifa iliyotolewa mnamo Novemba 23, Andrew Nkea, ambaye pia ni mkuu wa Baraza la Maaskofu nchini Cameroo, aliwasihi wafanyakazi wa kidini katika eneo lililoathiriwa kujiandaa kuondoka, kutokana na ukosefu wa dhamana za usalama.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Utekaji nyara wa mapadri na wamishonari wetu unatulazimisha kuchukua hatua kali,” ametangaza Askofu Mkuu Andrew Nkea. Siku kumi zilizopita, Jumamosi, Novemba 15, kasisi na msaidizi wake walitekwa nyara huko Baba I, katika wilaya ya Babessi, na wanaume wanaodai kuwa wapiganaji wanaotaka kujitenga kwa eneo lao, kulingana na taarifa kutoka kwa viongozi wa kidini huko Bamenda, Kaskazini Magharibi mwa Cameroon.

Siku tatu zilipita, na Jumanne, Novemba 18, mapadri wanne na kasisi walijaribu kujadiliana na watekaji nyara na wao wenyewe walikamatwa. Siku mbili baadaye, wote waliachiliwa isipokuwa mmoja: Padre John, ambapo watekaji nyara waliomba fidia. “Kanisa halilipi kamwe,” taarifa hiyo imekumbusha

Ikiwa Padre John hataachiliwa ifikapo kesho, Askofu Mkuu wa Bamenda aliwaamuru mapadri na wafanyakazi wa kidini wa dekani ya Ndop kuondoka, wakifunga parokia na shule hadi taarifa zaidi itakapotolewa. Mapadri waliagizwa kuondoa Sakramenti Takatifu kutoka makanisani.

Askofu amehalalisha hatua hii kwa kusema kwamba usalama wa mapadri na wafanyakazi wa kidini hauzingatiwi katika eneo hilo. Na siku ya Ijumaa, Novemba 28, ikiwa Padre John atakuwa bado kizuizini, askofu mkuu anaahidi kwenda mwenyewe na wafanyakazi wa kidini na walei katika eneo hilo hadi mateka huyo alipo.

“Watu wa maeneo ya Kaskazini Magharibi na Kusini Magharibi wameteseka vya kutosha.” Askofu mkuu anatoa wito kwa jeshi kuhakikisha usalama kwa weledi na maadili. Anarejelea wito wake wa mazungumzo ili kukomesha mgogoro katika maeneo mawili yanayozungumza Kiingereza nchini, ambao sasa unaingia mwaka wake wa tisa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *