
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron leo Jumanne, Novemba 25, kwenye redio ya RTL, ametoa wito wa kutoonyesha “udhaifu” mbele ya “tishio” kutoka Urusi, ambayo ina “msimamo mkali zaidi,” shirika la habari la AFP limeripoti.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Rais wa Ufaransa amezungumza kwa kirefu kuhusu mzozo wa Urusi na Ukraine na akasema kwamba hakuna suala la “kuwatuma vijana wetu Ukraine.”
Je, vita nchini Ukraine vitapata suluhu hivi karibuni? Karibu miaka minne baada ya kuanza kwa mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine, mazungumzo kati ya Kyiv na Washington yanafanyika wiki hii ili kujaribu kupata maelewano na kukomesha mzozo huo. Akihojiwa Jumanne asubuhi na wenzetu wa kituo cha RTL, Rais Emmanuel Macron alitaka “kutoonyesha udhaifu” mbele ya “tishio” kutoka Urusi.
“Tutakuwa tumekosea kuwa dhaifu mbele ya tishio hili. Na kwa hivyo, ikiwa tunataka kujilinda, sisi Wafaransa, mtazamo wangu pekee wa kushinda, lazima tuonyeshe kwamba hatuko dhaifu mbele ya taifa linalotutishia zaidi,” amesema mkuu wa nchi, ambaye atashiriki leo alasiri katika mkutano kwa njia ya video wa muungano wa nchi zinazounga mkono Ukraine.