Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limeonya kuwa mashambulio ya makundi ya wanajihadi na ukosefu wa uthabiti kaskazini mwa Nigeria yanasababisha viwango vya baa la njaa kuongezeka.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Kulingana na WFP, karibia watu Milioni 35 wanatarajiwa kukabiliwa na uhaba wa chakula mwaka ujao wa 2026.

Katika jimbo la Borno, kitovu cha mzozo wa miaka 16 sasa, karibia watu Elfu 15 wanatarajiwa kukabiliwa na baa la njaa au dalili kulingana na WFP.

Mzozo wa kaskazini mwa Nigeria umesababisha vifo vya zaidi ya watu Elfu 40 wakati wengine Milioni 2 kaskazini mashariki mwa nchi wakipoteza makazi yao, mzozo ambao hata hivyo umeingia hadi katika mataifa jirani.

Shule ya wasichana katika eneo la Kebbi nchini Nigeria ambako watu wenye silaha waliteka wanafunzi na Walimu.
Shule ya wasichana katika eneo la Kebbi nchini Nigeria ambako watu wenye silaha waliteka wanafunzi na Walimu. AIT via REUTERS – Africa Independent Television

Kando na kuwepo kwa kundi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria, taifa hilo la Afrika Magharibi pia linakabiliwa na utovu mwengine wa usalama unaosababishwa na makundi mengine ya wapiganaji katikati mwa nchi na hata Kaskazini Magharibi.

Makundi hayo yenye silaha yamekuwa yakitekeleza mashambulio katika vijiji tofauti kwenye maeneo hayo wakitekeleza mauaji ya raia na hata kuwateka wengine yakiwa na nia ya kulipwa fidia.

Wiki iliopita, Nigeria yenye idadi kubwa ya watu barani Afrika iliripoti matukio matatu ya utekaji wa watu.

Watu wenye silaha walitekeleza shambulio dhidi ya shule na kanisa nchini Nigeria wiki hii.
Watu wenye silaha walitekeleza shambulio dhidi ya shule na kanisa nchini Nigeria wiki hii. REUTERS – Abdullahi Dare Akogun

Zaidi ya wanafunzi 300 na Walimu wao walitekwa kutoka katika shule inayomilikwa na kanisa Katoliki katika jimbo la Niger.

Katika tukio lengine, wanafunzi 25 wa kike walitekwa kutoka katika shule nyengine jirani katika jimbo la Kebbi.

Wahuni 38 walitekwa wakati wakiendelea na ibaada yao iliyokuwa ikiperushwa moja kwa moja katika jimbo la Kwara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *