Nchini Sudan, Abdel Fattah al-Burhan amekataa mpango mpya wa kusitisha mapigano uliopendekezwa na Marekani. Kamanda wa jeshi alitangaza hili siku ya Jumapili, Novemba 23, wakati wa hotuba kwa maafisa wake wa ngazi za juu. 

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu jijini Nairobi, Gaëlle Laleix

Wiki iliyopita, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kujitolea kwake kukomesha vita kati ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vya cha Jenerali Hemedti, hasa kupitia upatanishi wa “Quad,” kundi linalojumuisha Marekani, Saudi Arabia, Misri, na Falme za Kiarabu. Siku ya Jumatatu jioni, Jenerali Hemedti alitangaza kusitisha mapigano kwa miezi mitatu kwa upande mmoja.

Kulingana na mkuu wa jeshi la Sudan, Jenerali al-Burhan, “Pendekezo la kusitisha mapigano lililotolewa na mjumbe maalum wa Marekani kwa Afrika ndilo baya zaidi kuwahi kufanywa.”

Sio tu kwamba mpango wa Massad Boulos hautoi wito wa kuvunjwa kwa RSF, lakini kwa kweli unatoa wito wa kuvunjwa kwa jeshi na vyombo vya usalama vya serikali ya Port Sudan, pendekezo linaloonekana “halikubaliki” na Jenerali al-Burhan, ambaye anamshuku mjumbe wa Marekani kwa kuwa na upendeleo.

Kiini cha tatizo ni tuhuma za Washington kuhusu ushawishi mkubwa wa Muslim Brotherhood kwa jeshi la Sudan. Kwa mujibu wa Jenerali al-Burhan, matamshi haya ni propaganda kutoka Falme za Kiarabu, ambazo anazituhumu kuwa msaidizi mkuu wa RSF.

“Kuibuka tena kwa ushawishi wa Muslim Brotherhood [ni] sababu kubwa ya wasiwasi,” Anwar Gargash, Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Falme za Kiarabu,ameandika kwenye mtandao wa kijamii wa X.

“Kukataa kwa Burhan udhibiti wa kundi hili la wanamgambo wa Kiislamu kwa jeshi ni jaribio la kusikitisha la kudanganya jumuiya ya kimataifa,” ameongeza Elbasha Tibeig, mshauri wa Jenerali Hemedti, kamanda wa RSF.

Kwa Andreas Krieg, profesa katika Shule ya Masomo ya Usalama katika Chuo cha King’s London, “kampeni hii ya upotoshaji lazima ikomeshwe, na ushawishi wa Abu Dhabi lazima utumike kulazimisha kusitisha mapigano.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *