Kutokana na ripoti hiyo iliyotolewa leo Januari 28, 2026, takwimu zimeonesha zaidi ya wanawake wajawazito na wanaonyonyesha 219,000 nchini humo wamepata athari mbaya za utapiamlo kutokana na uhaba wa chakula na huduma duni za afya.

Hali hii imechochewa na mambo kadhaa nchini Chad ikiwemo ulaji duni wa chakula, kukosekana kwa aina mbalimbali za lishe kwa watoto, na milipuko ya magonjwa ya utotoni kama malaria na surua. Matatizo ya usafi wa mazingira, ukosefu wa maji safi, na ongezeko la wakimbizi kutokana na mzozo wa Sudan yamezidisha shinikizo kwenye rasilimali chache zilizopo. Takwimu zimeonyesha kuwa kiwango cha utapiamlo kimesalia katika hali ya Daraja la 3 na Daraja la 4 katika maeneo mengi ya nchi.

Hali bado inakadiriwa kuwa mbaya zaidi

Kati ya Juni na Septemba 2026, hali imetajwa kuwa itakuwa mbaya zaidi kutokana na msimu wa kilele wa utapiamlo. Wakati huohuo, juhudi za Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa na wadau wake zimeelekezwa katika kuimarisha ufuatiliaji wa lishe na kusambaza dawa kabla ya msimu wa mvua kuanza.

Bila hatua za makusudi za kuimarisha mifumo ya lishe na usafi, idadi ya vifo na magonjwa itazidi kuongezeka nchini kote. Juhudi za Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa na wadau wa maendeleo zimehusisha kuimarisha uwezo wa jamii kujikinga, kutoa msaada wa fedha, na kukuza kilimo stahimilivu huku uwepo wa amani na utulivu wa kisiasa umeelezwa kuwa ndio suluhu ya kudumu itakayopunguza mahitaji haya makubwa ya kibinadamu na kuzuia hali ya utapiamlo isizidi kuwa mbaya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *