Kiongozi wa Guinea-Bissau, Jenerali Horta N’Tam, amepandishwa cheo cha meja jenerali — cheo cha juu kabisa katika vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo, kulingana na amri aliyoiweka saini na kutangazwa Alhamisi.

Jeshi lilichukua madaraka Novemba iliyopita, siku chache tu baada ya uchaguzi wa urais wa nchi hiyo, likamuondoa madarakani rais wa zamani Umaro Sissoco Embalo na kusitisha mchakato wa uchaguzi.

Awali, jeshi lilisema litachukua udhibiti kwa muda wa mwaka mmoja na kumteua N’Tam — mshirika wa karibu wa Embalo — kuwa rais wa mpito.

Mpaka sasa, Disemba 6, 2026 ndio imetengwa kuwa siku ya uchaguzi wa urais na wa bunge, unaokusudiwa kurudisha madaraka kwa raia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *