Kim Jong-un anatafuta kuimarisha mstari wa mbele dhidi ya ‘adui yake mkuu’ Korea KusiniKim Jong-un anatafuta kuimarisha mstari wa mbele dhidi ya ‘adui yake mkuu’ Korea Kusini

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametoa wito wa kuimarisha vitengo vya kijeshi vya mstari wa mbele dhidi ya “adui wake mkuu, Korea Kusini,” shirika la habari la serikali, KCNA, limeripoti leo Jumatatu, Mei 18.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Kim Jong-un “amewasilisha mipango ya kuimarisha vitengo vya mstari wa mbele na vitengo vingine vikubwa kijeshi na kiufundi” ili kuongeza uwezo wake wa “kuzuia”, kulingana na taarifa ya KCNA. “Amebainisha kwamba makamanda katika ngazi zote za jeshi lazima waendelee kuboresha uelewa wao wa adui mkuu,” ripoti hiyo imeongeza, ikimaanisha wazi Korea Kusini.

Nchi hizo mbili jirani bado ziko vitani tangu mzozo wao wa mwaka 1950-1953, ambao ulimalizika kwa makubaliano ya kusitisha mapigano, na sio mkataba wa amani. Licha ya ishara za upatanishi za rais wa Korea Kusini aliyechaguliwa mwaka jana, Pyongyang inakataa kimfumo makubaliano ya Seoul.

Kim Jong-un pia ametaja sera ya serikali ya “ulinzi wa eneo kuhusu uimarishaji wa vitengo vya mstari wa mbele kwenye mpaka wa kusini na mabadiliko ya mstari wa mpaka kuwa ngome isiyoweza kuingiliwa.”

Nafasi adimu iliyo wazi katika sekta ya michezo

Kwa Hong Min, mchambuzi katika Taasisi ya Korea kwa ajili Umoja wa Kitaifa, taarifa hii inaonyesha masomo yaliyopatikana kutokana na vita vilivyoanzishwa na Urusi dhidi ya Ukraine, ambapo Pyongyang iliunga mkono Moscow kwa kutuma wanajeshi. “Taarifa hii inaonyesha ufahamu wa mbinu za vita vya droni, mashambulizi ya usahihi, vita vya kielektroniki, na viwanja vya vita vya nyanja nyingi (katika maeneo mengi) vilivyoonekana wakati wa vita nchini Ukraine” na Mashariki ya Kati, ameliambia shirika la hbari la AFP.

Licha ya tangazo hili la hivi karibuni la ongezeko la uhasama, mwanga mdogo wa matumaini umeonekana kwa kuwasili nchini Korea Kusini kwa timu ya mpira wa miguu ya wanawake ya Korea Kaskazini siku ya Jumapili. Ziara kama hiyo ya michezo haikuwahi kutokea kwa karibu miaka minane.

Naegohyang FC itakabiliana na Suwon FC ya Korea Kusini siku ya Jumatano katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa ya Asia katika mechi iliyoisha. Vyama vya Korea Kusini, vinavyofadhiliwa na Seoul, vinapanga kuziunga mkono timu zote mbili, kwani mashabiki wa Korea Kaskazini wamepigwa marufuku kuvuka mpaka.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *