
Ajali kati ya basi dogo na lori imesababisha fivo vya watu 13 siku ya Alhamisi, Mei 28, 2026, katikati mwa China, televisheni ya serikali imeripoti. Basi dogo, lililoidhinishwa kubeba abiria tisa lakini ilikuwa na watu 16, liligonga nyuma lori lililokuwa likisafiri mbele yake usiku kwenye barabara kuu huko Nanyang, mkoa wa Henan, televisheni hiyo imeripoti. Watu watatu pia wamejeruhiwa katika ajali hiyo.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Idara ya uchukuzi katika Wizara ya Usalama wa Umma imesema kwenye mitandao ya kijamii kuwa ajali hiyo imesababisha vifo vya watu kumi na tatu na watatu wamejeruhiwa huko Nanyang, Mkoa wa Henan. Watu watatu walijeruhiwa katika ajali hiyo.
Wizara imetuma timu mara moja kwenye eneo la tukio ili “kusimamia uchunguzi na kudhibiti hali hiyo,” iidara hiyo imesema katika taarifa.
