
Katika hotuba iliyorushwa kwenye televisheni siku ya Ijumaa, Juni 12, Rais wa Nigeria Bola Tinubu amedai kwamba “zaidi ya magaidi 13,000” wameuawa na jeshi katika mwaka uliopita na kwamba idadi ya waathiriwa wa uasi wa wanajihadi nchini imepungua kwa 81% tangu alipoingia madarakani mwaka wa 2023. Wachambuzi wanaonya kwamba takwimu hizi zinapaswa kuchukuliwa kwa tahadhari kubwa, kwani zinaonekana “zisizoaminika.”
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Kwa kuwa uchaguzi mkuu unakaribia, mwezi Januari 2027, hali ya usalama iko katikati ya matarajio na mijadala nchini Nigeria kuliko wakati mwingine wowote. Katika hotuba iliyorushwa kwenye televisheni, Rais Bola Tinubu, siku ya Ijumaa Juni 12, alitumia fursa ya sikukuu ya kitaifa ya kuadhimisha ujio wa demokrasia mwaka wa 1999, kutoa tathmini chanya ya rekodi yake katika suala la usalama.
Akidai kwamba “zaidi ya magaidi 13,000” wameuawa na jeshi katika mwaka uliopita, pia alisema kwamba idadi ya waathiriwa wa uasi wa wanajihadi nchini Nigeria imepungua kwa 81% tangu alipoingia madarakani mwaka wa 2023.
Hata hivyo, kauli hizi zinapaswa kuchukuliwa kwa tahadhari. Kulingana na mchambuzi aliyeko Abuja, takwimu zilizowasilishwa na mkuu wa nchi zinaonekana “zisizoaminika.” “Hakuna uhakika kwamba hawa ni magaidi: takwimu hizi zinaweza kujumuisha raia walionaswa katika mapigano,” anaelezea, pia akisema kwamba “makundi yenye silaha yameongezeka tangu Bola Tinubu alipoingia madarakani zaidi ya miaka mitatu iliyopita” na kwamba “idadi ya waathiriwa imeongezeka sana.”
Athari ndogo
“Ni kweli kwamba serikali hii imewaua viongozi kadhaa wa wanajihadi au viongozi wasio na itikadi,” mchambui huyu anaongeza, lakini shughuli hizi “zina athari ndogo tu” mradi tu uajiri unaendelea na makundi haya yanaendelea kutafuta njia za kujipatia fedha. Kwa upande mwingine, anabainisha kwamba “wapiganaji 124,000 na washirika wao” wameweka silaha zao chini tangu mwaka 2023, kutokana na mpango wa kuondoa msimamo mkali wa Safe Corridor uliotekelezwa katika jimbo la Borno.
Wakati Bola Tinubu alikuwa akijipongeza kwa rekodi yake, raia wenye hasira walikuwa wakiandaa maandamano huko Lagos na Abuja kukemea hali ya uchumi na usalama inayozidi kuzorota.