Chanzo cha picha, Images
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 6
Nyimbo za Kombe la Dunia zinaweza kuwa mojawapo ya nguzo rasmi za mchuano huo, na ndizo njia za kusisimua zaidi za kuleta shauku ya umma kabla ya kuanza kwa toleo lolote la shindano.
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) huchagua wimbo rasmi wa mashindano, na imekuwa kawaida katika matoleo machache ya mwisho ya Kombe la Dunia kupitisha zaidi ya wimbo mmoja, wa kwanza ambao hutumika kama wimbo rasmi wa mashindano, pamoja na wimbo wa pili au wa tatu, na wakati mwingine hata albamu nzima chini ya makundi na majina tofauti ili kukuza tukio kubwa la michezo duniani.
Ingawa nyimbo zilizopitishwa rasmi na FIFA na kupendwa sana zilikuwa chache, waimbaji kadhaa pia walikuwa wakitoa nyimbo kuhusu soka na mashindano kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia, hata bila FIFA kupitisha nyimbo hizi.
Wimbo wa kwanza wa Kombe la Dunia
Chanzo cha picha, Getty Images
Toleo la kwanza la Kombe la Dunia liliandaliwa na FIFA mnamo 1930, na mashindano hayakuhusishwa na wimbo usio rasmi hadi 1962, ilipofanyika Chile na kikundi cha muziki cha Chile kiliamua kuunda wimbo wa kusherehekea hafla hiyo.
Wimbo wa Chile uliotolewa kwa Kombe la Dunia wakati huo bado unashikilia rekodi ya kihistoria ya nakala nyingi zaidi zilizowahi kuuzwa nchini.
“El Roc del Mondial” (Mwamba wa Kombe la Dunia) na bendi ya Chile “Los Ramblers” ilirekodiwa Machi mwaka huo. Michuano hiyo ilianza Mei 30 na kumalizika Juni 17, 1962, ambapo Barzil waliibuka washindi.
Wimbo huu unachukuliwa kuwa wimbo wa kwanza rasmi katika Kombe la Dunia, lakini haukuwa wimbo rasmi ulioidhinishwa na FIFA kama ilivyo leo.
Wimbo huu ni wa aina ya rock na roll na mguso wa jazz, na umejaa nguvu. Muziki wa rock na roll ulikuwa ukienea sehemu nyingi za dunia wakati huo, ikiwemo Amerika Kusini.
Mwimbaji mkuu wa bendi hiyo, Herman Casas, aliimba wimbo huo kwa mtindo wa Elvis Presley katika kilele cha kazi yake, na kuupa wimbo wa Chile kwa Kihispania nyongeza ya mafanikio.
Maneno ya wimbo huo yanasema: “Kombe la Dunia la 1962 ni sherehe ya kimataifa ya michezo na soka. Na katika kusherehekea ushindi wetu, tutacheza kwa nyimbo za rock and roll.”
Anaongeza katika kifungu kingine: “Tutazionyesha timu za kigeni hisia zetu za ucheshi. Na kama Wachile wazuri, tutaonyesha uungwana na uungwana. Na hata tukishindwa, tutacheza kwa nyimbo za rock na roll.”
Wimbo huo unaendelea: “Chukua faida, weka mpira ndani, umekwisha! Goli, goli kwa Chile! Let’s rock ‘n’ roll!”
Wimbo huo tangu wakati huo umekuwa wimbo usio rasmi kwa timu ya taifa ya Chile, na wengine wanasema huenda umeisaidia timu hiyo kufikia nafasi ya mshindi wa tatu kaika ardhi ya nyumbani, mafanikio ya kihistoria.
Chanzo cha picha, Getty Images
Wanahistoria wengine pia wanaamini kuwa wimbo huu ndio ulizindua wazo la kupitisha wimbo rasmi wa Kombe la Dunia.
Kituo hicho kiliongeza kuwa baada ya muda, wimbo huo ukawa “wimbo wa pili wa taifa,” kwani ulitangazwa kwenye “kila kituo cha redio, kila nyumba, wakati wote.”
Wimbo huo pia ulipata umaarufu mkubwa katika nchi zingine za Amerika Kusini.
Tangu wakati huo, cheche za nyimbo za Kombe la Dunia zimeenea, na kila toleo lililofuata limekuwa na wimbo rasmi, unaohusishwa kwa njia moja au nyingine na nchi inayoandaa mashindano.
Wimbo wa kwanza kutayarishwa kwa Kombe la Dunia, ulioidhinishwa na FIFA yenyewe, ulikuwa wimbo wa Kombe la Dunia la 1990 nchini Italia.
Maneno ya “Unni Stati Italiana” au “Majira ya Kiitaliano” na Edoardo Bennato na Gianna Nannini, wimbo wa pop-rock, wanasema: “Ndoto hizo ambazo huanza utotoni na daima zinakupeleka mbali zaidi, sio hadithi kutoka kwenye vyumba vya kubadilisha, vijana hutoka nje, tunafanya bidii kila siku tukijitahidi kufikia lengo la majira ya joto la Italia.”
Wimbo huo ulipata mafanikio makubwa nchini Italia na nchi nyingine za Ulaya, zikiwemo Uswisi, Ujerumani, Norway na Uswidi.
“Kombe la Maisha”
Chanzo cha picha, Getty Images
Waimbaji wa Kilatini walikuwa na jukumu muhimu katika umaarufu wa nyimbo za Kombe la Dunia.
Baada ya kuzinduliwa kwa wimbo wa kwanza wa “nusu-rasmi” wa Kombe la Dunia kutoka Chile, Ricky Martin wa Puerto Rico, miaka 36 baadaye, alikuwa na wimbo wa kwanza “uliotamba dunia nzima” katika Kombe la Dunia.
Kwa Kombe la Dunia la 1998 nchini Ufaransa, FIFA ilipitisha nyimbo mbili rasmi. Ya kwanza, kwa Kifaransa, lugha ya nchi mwenyeji, ilichezwa na mwimbaji wa Senegal na mwimbaji wa Ubelgiji na iliitwa wimbo rasmi. Ya pili ilikuwa “wimbo rasmi” wa Ricky Martin, ambaye alirekodi matoleo mawili, moja kwa Kihispania na nyingine kwa Kiingereza, ambayo yote yalijumuisha neno “allez” au “Hala” kwa Kifaransa.
Wimbo huo unaochanganya miondoko ya samba na miondoko ya pop ya Kilatini, ilipata mafanikio ya kuvunja rekodi katika nchi mbalimbali duniani wakati huo na kubaki maarufu .
Chanzo cha picha, Getty Images
“La Copa de la Vida” (Kombe la Maisha) ilibadilisha kabisa njia ya kazi ya Martin, na kumfanya kuwa mmoja wa waimbaji maarufu zaidi ulimwenguni. Pia alishinda Tuzo ya Grammy ya Utendaji Bora wa Kilatini wa Pop kwa wimbo huu.
Kazi hii inachukuliwa kuwa hatua ya kugeuza sio tu katika kazi ya Martin, lakini katika muziki wa Kilatini ulimwenguni kote, na wimbo huu unapewa sifa ya kuunda “mlipuko wa Kilatini”.
Kwa kushangaza, cheche za muziki wa Kilatini na mafanikio ya wimbo huu yalifikia ulimwengu wa siasa. Ricky Martin alialikwa kutumbuiza katika sherehe za kuapishwa kwa Rais George W. Bush Januari 18, 2001. Martin alitoa onyesho la wimbo huo kwa shauku, na kumfanya rais mteule, Bush, kuungana naye jukwaani kucheza dansi.
Martin alikabiliwa na ukosoaji mkubwa na vikali kwa ushiriki wake katika sherehe ya kuapishwa kwa sababu ya utawala wa kihafidhina wa Bush. Mzozo huo ulizidi miaka mingi baadaye wakati Martin alipofanya ishara chafu kuelekea rais huyo wa zamani wakati wa tamasha.
Hata hivyo, Martin alimkosoa tena Bush kwa njia chafu wakati wa tamasha huko Mexico mwaka wa 2007, baadaye akielezea kama kulaani vita vya Bush nchini Iraq.
“Waka Waka (Wakati huu kwa Afrika)”
Chanzo cha picha, Getty Images
Inaweza kusemwa kuwa karibu haiwezekani kwa mtu yeyote ulimwenguni leo kutojua wimbo rasmi wa Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini na mwimbaji wa Colombia Shakira, unaoitwa: “Waka Waka”.
Wimbo huu unatumia kionjo cha wimbo maarufu wa Cameroon wa mwaka 1986 uitwao “Zamina Mena,” wimbo unaohusu wanajeshi waliopigana, ambapo Shakira alitumia maneno haya: “Haya, njoo, unatoka wapi? Njoo mbele, njoo mbele.”
Shakira anaimba kwa Kiingereza: “Wewe ni mwanajeshi shujaa, unachagua vita vyako vizuri. Inuka tena, utimue vumbi, na urudi uwanjani. Uko mstari wa mbele, na macho yote yako kwako. Unajua ni mbaya, tunakaribia, lakini bado haijaisha.”
Video ya muziki inayowashirikisha Cristiano Ronaldo na Lionel Messi imetazamwa zaidi ya bilioni 4.5 kwenye YouTube na, hadi tunapoandika, imeorodheshwa ya 14 kwenye orodha ya video za muziki zilizotazamwa zaidi kwenye YouTube ulimwenguni kote.
Wimbo huo ulipata mitiririko wa 1,074,458,645 kwenye Spotify kufikia Januari 13, 2025, na kuifanya kuwa Rekodi ya Dunia ya Guinness kwa wimbo uliotiririshwa zaidi wa Kombe la Dunia la FIFA kwenye Spotify.
‘Ole Ole’
Chanzo cha picha, GETTY
Sio nyimbo zote rasmi za FIFA za Kombe la Dunia zimefikia kiwango sawa cha umaarufu.
Katika Kombe la Dunia la 2014 nchini Brazili, mwimbaji wa Cuba-Amerika Pitbull, mwimbaji wa Puerto Rican-Amerika Jennifer Lopez na nyota wa Brazil Claudia Leitte walishirikiana kwenye wimbo rasmi “Olé Olah (We Are One),” wimbo wa samba wa lugha tatu (Kiingereza, Kihispania na Kireno).
Maneno ya wimbo huo yanasema: “Inueni bendera zenu juu (ziinue juu), zipeperushe kulia na kushoto, onyesha ulimwengu ulikotoka, onyesha ulimwengu kuwa sisi ni wamoja (mmoja, upendo, maisha).”
Wimbo huo mwanzoni ulikabiliwa na hisia hasi kutoka kwa Wabrazil, kutokana na kutokuwa na mhusika wa Kibrazili katika bossa nova au samba, na baadhi waliuchukulia muziki wa wimbo huo kuwa “muziki wa pop sawa na nyimbo nyingine nyingi, za kuchosha na za kawaida.”
Toleo jingine la wimbo huo lilitolewa baadaye, likiwa na mabadiliko kidogo ya muziki, baada ya bendi ya Brazil ya Olodum, inayojulikana kwa miondoko yao halisi ya Kibrazili, kualikwa kushiriki. Toleo la Olodum lilitumika katika video yao ya muziki.