Mahakama ya Afrika Kusini siku ya Alhamisi, Juni 18, ilimtoza faini mratibu wa msafara wa kitalii randi milioni mbili, au karibu dola 123,000, aliyeelezewa kama kiongozi mkuu wa kundi kubwa la biashara ya pembe za faru kimataifa. Uamuzi huu unahitimisha kesi iliyoanza mwaka wa 2010 na iligubikwa na ucheleweshaji mwingi na rufaa za kisheria.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Afrika Kusini, ambayo kuna faru wengi ambao bado wako hai, ni mojawapo ya vituo vikuu vya ujangili wa faru. Huko Asia, pembe za faru huuzwa bei kubwa kutoka kwa wanunuzi ambao wanaamini kimakosa kwamba zina faida za kiafya”. Kwa hivyo, mahakama haikusita katika uamuzi wake dhidi ya mratibu wa msafara wa kitalii  ambaye alipanga operesheni nzima ya usafirishaji haramu wa kimataifa.

Ulaghai, utakatishaji fedha, uwindaji haramu, na kuondoa pembe za faru: zaidi ya mashtaka 1,700 yaliwasilishwa dhidi ya mshukiwa mkuu na washtakiwa wenzake katika kesi “iliyochukuliwa kuwa uchunguzi mkubwa zaidi duniani kuhusu biashara haramu ya pembe za faru.”

Kulingana na ripoti iliyochapishwa mwaka wa 2014 na Wizara ya Sheria ya Marekani, mratibu huyu wa msafara wa kitalii ndiye aliyekuwa kiongoezi mkuu wa operesheni ya biashara haramu. Aliuza safari kwa wawindaji haramu kwa minajili ya kwenda kuwinda faru

Kesi hiyo, iliyoanza mwaka wa 2010, hatimaye ilimalizika Alhamisi, Juni 18, 2026, kwa makubaliano ya kukiri mashtaka kati ya mshtakiwa na mwendesha mashtaka wa Afrika Kusini, na kusababisha faini badala ya hatia: randi milioni mbili, au karibu dola 123,000.

Kulingana na Wakfu wa Kimataifa wa faru, idadi ya faru weupe barani Afrika ilipungua na kuwa 16,000 mwaka wa 2025. Faru weusi, walioainishwa kama walio hatarini kutoweka, wanapata nafuu na sasa wanafikia takriban 6,800 katika bara la Afrika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *