Watabiri wa hali ya hewa nchini Marekani (NWS) wameendelea kutoa tahadhari ya wimbi la joto la muda mrefu na hatari ambalo litaathiri eneo kubwa la nchi hiyo kuanzia pwani ya mashariki ya Marekani hadi maeneo ya kati kuanzia siku ya Alhamisi.
Maafisa wanawaonya watu wanaoishi katika maeneo yaliyoathiriwa kupunguza muda wa kukaa nje, kukaa na maji mengi na kuhakikisha upatikanaji wa vituo vya kiyoyozi au vya kupoeza huku Meya wa Jiji la New York Zohran Mamdani akianzisha mpango wa dharura wa joto huku mamia ya vituo vya kupoeza vikitarajiwa kufunguliwa kote jijini humo.
Shirika la Afya Duniani WHO linasema wimbi hilo linakuja baada ya joto la mapema la kiangazi barani Ulaya kuteketeza nchi kadhaa katika siku za hivi karibuni, huku rekodi za halijoto zikivunjwa kwa kusababisha vifo 1,300, ambako kwa upande wa Ujerumani joto limefika nyuzi joto 41.7C, Canada nyuzi joto 37C hadi Ontario.

(Feed generated with FetchRSS)