- Lionel Messi alibubujikwa na machozi baada ya Argentina kutoka nyuma na kuifunga Misri na kutinga robo fainali ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 Jumanne, Julai 7
- Messi alikuwa amekosa penalti katika kipindi cha kwanza huku Misri ikitangulia kwa mabao 2-0 na kutishia kuandika moja ya matokeo ya kushangaza zaidi katika historia ya Kombe la Dunia
- Nyota huyo wa Argentina alianza kurejesha matumaini ya timu yake kwa kufunga bao moja na kutoa pasi ya bao, kabla ya kukiri kuwa alihisi amewaangusha wenzake hadi Mungu alipomuingilia kati
Lionel Messi alionekana akilia uwanjani baada ya Argentina kufanya comeback ya kushangaza dhidi ya Misri katika Kombe la Dunia la FIFA 2026, na sasa nyota huyo mwenyewe ameeleza kwa nini aliguswa sana kihisia.

Source: Getty Images
Argentina ilijikuta ikikaribia kuondolewa mapema baada ya Misri kutangulia kwa mabao 2-0, huku Messi akiwa tayari amekosa penalti katika kipindi cha kwanza. Kwa muda, ilionekana mabingwa watetezi walikuwa wakielekea kurejea nyumbani.

Pia soma
Kwa nini kocha wa Misri alionyesha ishara ya X? Kilichotokea baada ya comeback ya Argentina
Badala yake, kilichofuata kilikuwa mojawapo ya comeback za kusisimua zaidi katika historia ya Kombe la Dunia.
Messi alianza kurejesha matumaini ya Argentina kwa kufunga bao moja na kutoa pasi ya bao, akiisaidia timu yake kurejea na kushinda mechi hiyo ili kujihakikishia nafasi ya kucheza robo fainali.
Filimbi ya mwisho ilipopulizwa, nyota huyo mwenye umri wa miaka 39 alionekana amezidiwa na hisia na kububujikwa na machozi uwanjani.
Kwa nini Messi alilia baada ya mechi?
Akizungumza baada ya mchezo, Messi alieleza wazi uzito wa hisia aliokuwa nazo wakati wa mechi.
“Nililia kwa sababu nilihisi kwamba nimewaangusha wenzangu kutokana na penalti niliyokosa… na namna nilivyoipiga. Lakini namshukuru Mungu, kwa mara nyingine tena alikuwa amenitunzia jambo maalum mwishoni. Nina furaha sana,” alisema.
Ilikuwa ni moja ya nyakati nadra ambazo zilionyesha hisia halisi za mmoja wa wachezaji waliotwaa mataji mengi zaidi katika historia ya soka, mtu ambaye ameona kila kitu ambacho mchezo huu unaweza kutoa, lakini bado akabubujikwa na machozi kwa kuhofia kuwa ameangusha timu yake.
Kutoka ukingoni mwa kuondolewa hadi robo fainali

Pia soma
WC 2026: Kwa nini bao la enzo Fernandez katika mechi ya Argentina vs Misri lilipaswa kukataliwa
Machozi ya Messi baada ya filimbi ya mwisho yamejadiliwa sana, huku wengi wakisema yanaonyesha jinsi anavyoendelea kuhisi uzito mkubwa wa jukumu la kuiongoza nchi yake hata katika hatua hii ya mwisho ya maisha yake ya soka.
Mlolongo wa matukio uliifanya comeback hiyo kuwa ya kipekee zaidi. Messi alikosa penalti, Misri ikaadhibu Argentina kwa mabao mawili na kutangulia 2-0, huku dunia ikianza kujiuliza kama huo ndio ungekuwa mwisho wa safari yake katika Kombe la Dunia.
Badala yake, Messi alibadilisha mchezo kwa juhudi zake binafsi na kuonyesha tena roho ya kutokata tamaa ambayo Argentina imekuwa ikijulikana nayo.
Sasa Argentina itaanza maandalizi ya robo fainali, huku Messi akithibitisha kwa mara nyingine kuwa simulizi yake katika mashindano makubwa zaidi ya soka bado haijafikia mwisho.

Source: Getty Images
Kwa nini bao la Enzo Fernandez dhidi ya Misri lilipaswa kufutwa?
Pia tuliangazia ukweli kuhusu bao la utata la dakika za mwisho lililofungwa na Enzo Fernandez dhidi ya Misri katika Kombe la Dunia la FIFA 2026.
Argentina ilipokuwa ikijaribu kurejea kutoka nyuma baada ya kuwa imefungwa mabao 2-0, bao hilo lilizua mjadala mkubwa kuhusu haki katika maamuzi ya waamuzi, hasa kutokana na maamuzi tofauti ya VAR yaliyoshuhudiwa wakati wa mechi hiyo.
Makala haya yamedhaminiwa kwa fahari na 1xBet.
Read: ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke
